Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Korea Kusini yaonya kuharibu mji mkuu wa K Kaskazini
Maafisa wa Serikali ya Korea Kusini wamefichua kuwa serikali ina mipango ya kuharibu kabisa mji mkuu wa Korea kaskazini, iwapo ishara yo yote itaonekana kuwa kuna mipango ya kushambuliwa kwa nukilia.
Shirika la Habari la Yonhap lililo na uhusiano mkubwa na Korea Kusini linasema kwamba wabunge nchini humo wamepewa mpango huo.
Mpango huo unanuia kuharibu kabisha makombora yote yaliyo na zana hatari kukiwemo nukilia.
Ufichuzi huu unatokea siku mbili baada ya Korea Kaskazini kulipua angani jaribio kubwa zaidi la kinukilia, ambalo limetoa dhana kuwa Korea Kaskazini imepiga hatua kubwa katika utengenezaji wa zana za kinukilia.