Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Umoja wa Mataifa kuiwekea Korea Kaskazini vikwazo
Baraza la usalama la umoja wa mataifa linatarajiwa kuanza kuweka vikwazo mpya dhidi ya Korea Kaskazini katika kujibu jaribio la silaha za kinyuklia lililotekelezwa na Pyongyang.
Korea kusini inasema itahimiza kuwekwa kwa vikwazo dhabiti ili kuizuia Korea Kaskazini.
Serikali za Marekani na korea kusini zimeanza kufanya uchunguzi wa hewa na bahari kuchunguza athari ya vifaa vya mionzi vilivyotumika katika jaribio hilo, na kubaini ni silaha gani iliyofanyiwa majaribio.
Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa lilikutana na kutoa taarifa ya kuikosoa vikali majaribio hayo ya Korea Kaskazini.