Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Beyonce atawala tuzo za MTV Marekani
Mwanamuziki wa Marekani Beyonce alitawala tuzo za muziki za MTV mjini New York siku ya Jumapili akijipatia mataji saba.
Msanii huyo alijishindia tuzo kubwa katika tamasha hilo kwa kujishindia video ya mwaka kwa nyimbo yake 'Formation' ambayo inataja ubaguzi wa rangi,utumiaji wa nguvi kupitia kiasi unaofanywa na maafisa wa polisi pamoja na kimbunga Katrina.
Beyonce aliwasili katika tamasha hiyo na mama zao wanaume wanne Wamarekani weusi ambao vifo vyao vilizua hisia kali.
Msanii wa pili aliyeteuliwa katika tuzo hizo Adele hakujishindia kitu.
Msanii Rihanna alitunukiwa tuzo ya mchango wake katika usanii kufikia sasa akiwa na umri wa miaka 28 pekee.