Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Korea Kaskazini yamzungumzia balozi aliyekimbia nchi
Korea Kaskazini imemshutumu mwanabalozi wake aliyekimbilia Korea Kusini hivi karibuni, kwamba mhalifu.
Katika matamshi ya kwanza, tangu balozi huyo kukimbia, shirika la habari la Korea Kaskazini, lilimuelezea mwanabalozi huyo kuwa mtu duni kabisa.
Lilisema mkimbizi huyo alikuwa akichunguzwa kwa ubadhirifu wa mali ya taifa, na kuuza siri za nchi.
Awali juma hili, Korea Kusini ilitangaza kwamba Thae Yong-ho, ambaye alikuwa naibu balozi wa Korea Kaskazini mjini London, aliwasili Korea Kusini na familia yake.
Anafikiriwa kuwa mwanabalozi wa cheo cha juu kabisa wa Korea Kaskazini, kuwahi kukimbia.