Vitabu vilivyo hatari zaidi kuvisoma

Kitabu kikichomwa moto

Chanzo cha picha, Getty Images

Hekaya ya Vitabu vya Sibylline (maandishi ya mythological na kinabii ya Roma ya kale) inasema kwamba katika jiji moja mwanamke alijitolea kuwauzia watu vitabu 12 vyenye ujuzi na hekima yote ya ulimwengu, kwa bei ya juu sana.

Walikataa, wakiona pendekezo hilo kuwa la kipuuzi, kwa hiyo akateketeza nusu ya vitabu hivyo papo hapo na kutoa vingine sita kwa bei maradufu. Wananchi wakamcheka japo kwa woga kidogo.

Mwanamke huyo alivichoma moto vitabuo vitatu zaidi, akaviweka vinngine kwa uuzaji, lakini akaongeza bei mara mbili. Kwa mara nyingine tena alikataa kwa kusita - nyakati zilikuwa ngumu na maisha yalionekana kuwa magumu na magumu zaidi.

Mwishowe, kilibaki kitabu kimoja tu, ambacho raia walilipa bei isiyo ya kawaida ambayo mwanamke huyo alidai.

Sehemu ya kumi na mbili ya maarifa na hekima yote ulimwenguni. Vitabu vimejaa maarifa. Wao ndio wachavushaji wa akili zetu, wakieneza mawazo ambayo yanajizalisha yenyewe kwa wakati na nafasi.

Tunaelekea kusahau jinsi sifa za ukurasa au skrini hufanya zinavyowezesha mawasiliano kati ya ubongo wa kila mmoja, mwishoni mwa dunia au mwishoni mwa karne.

Vitabu ni, kama Stephen King alivyosema, "mazingaombwe ya kipekee ya kubebeka" - na kipengele cha kubebeka ni muhimu kama mazingaombwe.

Kitabu kinaweza kubebwa, kufichwa, kama ghala lako la maarifa (shajara ya mwanangu ina kufuli - sio lazima lakini ni muhimu sana).

Nguvu ya maneno yaliyo katika kitabu ni kubwa sana kiasi kwamba imekuwa desturi kwa muda mrefu kufuta baadhi ya maneno yake: kama laana katika riwaya za karne ya 19, au maneno hatari sana kuandikwa, kama vile jina la Mungu katika maandishi fulani ya kidini.

Nguvu ya vitabu

Hauhitaji Whatsapp
BBC Swahili sasa kwenye WhatsApp

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Bonyeza hapa kujiunga

Mwisho wa Whatsapp

Vitabu ni maarifa na maarifa ni nguvu, jambo ambalo huwafanya watu kuwa tishio kwa mamlaka, serikali na watawala ambao wanataka kuhodhi maarifa na kudhibiti fikra za raia wao.

Na njia ya ufanisi zaidi ya kutumia mamlaka hayo dhidi ya vitabu ni kuvifanya kuwa haramu. Kupiga marufuku vitabu kuna historia ndefu na ya kutisha, lakini haijafa: ni tasnia hai.

Septemba iliadhimisha kumbukumbu ya miaka 40 ya Wiki ya Vitabu Vilivyopigwa Marufuku, tukio la kila mwaka (lililokuzwa na Jumuiya ya Maktaba ya Marekani na Amnesty International) ambalo "huadhimisha uhuru wa kusoma".

Ilizinduliwa mwaka wa 1982 ili kukabiliana na upinzani unaokua kwa baadhi ya vitabu shuleni, maktaba na kwenye maduka ya vitabu.

Kwa namna fulani, lazima nivutiwe na nguvu na uangalifu wa wale wanaotaka kupiga marufuku vitabu leo: ilikuwa rahisi zaidi wakati huo.

Karne nyingi zilizopita, wakati idadi kubwa ya watu hawakuweza kusoma na hakukuwa na upatikanaji rahisi wa vitabu, ujuzi wao ungeweza kuwa mdogo kutokana na vyanzo vichache. Kwa mfano, kwa muda mrefu Kanisa Katoliki liliwakatisha tamaa watu kumiliki nakala zao za Biblia, na liliidhinisha tu tafsiri yake ya Kilatini, hivyo ni watu wachache wa kawaida tu walioweza kuisoma.

Hatua hii inaonekana ilikusudiwa kuwazuia walei kutafsiri vibaya neno la Mungu, lakini pia ilihakikisha kwamba hawakuweza kuhoji mamlaka ya viongozi wa Kanisa.

Ingawa viwango vya watu wanaojua kusoma na kuandika vilipanda, kama walivyofanya wakati Uingereza ilipoanzisha sheria za elimu mwishoni mwa karne ya 19, vitabu viliendelea kuwa ghali, hasa kazi za fasihi ya hali ya juu ambazo maneno na mawazo yake yalikuwa ya kudumu zaidi (na yanayoweza kuwa hatari zaidi).

Ni mpaka miaka ya 1930, wachapishaji wa vitabu vya Albatross na Vitabu vya Penguin, ambapo hadhira mpya iliweza kukidhi hamu yake ya vitabu bora kwa bei nafuu.

Lakini wakati huo huo, katazo la vitabu lilikuwa karibu kuchukua mkondo mpya wa maisha, sawa na vile wachunguzi watarajiwa walivyojaribu sana kuendana na kuenea kwa nakala mpya ambazo zilichochea mawazo mapya na yenye kusisimua kwa wasomaji.

Kinachoshangaza kuhusu kuenea kwa marufuku ya vitabu katika karne ya ishirini ni jinsi tamaa ya kudumisha uwongo huu wa "kujilinda" ilivyokuwa.

''Kupotoshwa akili''

Leo, serikali ya China, kwa mfano, inaendelea kutoa amri dhidi ya vitabu vya shule ambavyo "haviambatani na maadili (ya nchi) ya msingi ya ujamaa; ambayo yana maadili tofauti, mitazamo ya ulimwengu, na dhana za maisha ya upotovu", lugha rahisi ambayo inaweza kutumika kwa kitabu chochote ambacho mamlaka haikubaliani nacho kwa sababu yoyote ile. (Ingawa "wanafunzi hata hawaangalii kabisa," mwalimu mmoja aliona mnamo 2020 alipoondoa riwaya za George Orwell za "Shamba la Wanyama" na "1984" kwenye rafu za maktaba ya shule.)

Nchini Urusi, mkakati wa kupiga marufuku kitabu umekuwa jambo la umma.

Wakati wa enzi ya Soviet, serikali ilijaribu kudhibiti tabia ya kusoma ya raia wake, na vile vile maisha yao yote. Mnamo 1958, mwandishi na mshairi, Boris Pasternak alipokea Tuzo la Nobel la Fasihi kwa riwaya yake "Dokta Zhivago", ambayo ilikuwa imechapishwa nchini Italia mwaka mmoja uliotangulia, lakini sio nchini mwake. Tuzo hii iliwakasirisha sana viongozi wa Sovieti (vyombo vya habari rasmi viliita kazi hiyo " mbaya ya kisanii") kiasi kwamba alilazimika kukataa tuzo hiyo.

Serikali ilikichukia kitabu hicho kwa kile ambacho hakikuwamo - haikusifu Mapinduzi ya Urusi - na kwa kile ilichokifanya: kilikuwa na madokezo ya kidini na kusherehekea ujasiri wa mtu binafsi (CIA, ikihisi "thamani kubwa ya propaganda" ya"Daktari Zhivago", iliyopangwa ili iweze kuchapishwa nchini Urusi).

Boris Pasternak, hapa na mkewe na mtoto wake, alilazimishwa na mamlaka ya Soviet kukataa Tuzo la Nobel la Fasihi

Chanzo cha picha, Getty Images

Kupigwa marufuku kwa vitabu katika Umoja wa Kisovieti kulisababisha maendeleo ya samizdat - au maandishi binafsi - ambayo yanadaiwa kuendelea kuwepo, kwa mfano, mashairi ya Osip Mandelstam. Mwandishi mkaidi Vladimir Bukovsky alitoa muhtasari wa samizdat hivi: "Ninaiandika, ninaihariri, ninaidhibiti, ninaichapisha, na kuisambaza.

Vitabu vinapopigwa marufuku au watu wanapojaribu kuvipiga marufuku, hoja ni sawa na mahali pengine: ni suala la kuwalinda watu wa kawaida, ambao inaelezwa hawana akili za kutosha kupambanua , yatokanayo na mawazo potovfu. Nchini Uingereza, marufuku ya vitabu mara nyingi imekuwa chombo dhidi ya kile kinachoonekana kama maudhui ya ngono.

Kwa kawaida ni jaribio la kutumia nguvu ya kikatili ya sheria kusitisha mabadiliko ya kijamii: mbinu ambayo mara zote inashindwa, Sifa za waandishi wengi zimetetereka kutokana na kukimbia kwao na sheria chafu za Uingereza.

Kuyaweka mawazo kwenye uhalisia

Wakati huo huo nchini Marekani, ni aina ya heshima kwa nguvu ya kudumu ya vitabu na kwamba kuvipiga marufuku kunaendelea kuwa maarufu sana katika ulimwengu ambapo kila wimbi jipya la teknolojia, kuanzia kwenye televisheni hadi michezo ya video hadi mitandao ya kijamii, inaleta hofu kuwa "haifai "kimaudhui.

Shule ni msingi mzuri sana wa majaribio ya udhibiti, kwa sehemu ni kwa sababu kuelekeza ya mtoto inaonekana kuwa njia mwafaka ya kuondoa hatari zinazoonekana, lakini pia kwa sababu (tofauti na maduka ya vitabu) bodi za shule zina ushawishi fulani kwa jamii.

Mnamo 1982, mwaka ambao wiki ya vitabu Iliyopigwa marufuku ilianza, jaribio la udhibiti wa shule Shule ya Island Trees katika Jimbo la New York) lilienda hadi Mahakama Kuu.

Katika tukio hilo, uongozi wa shule ulisema kwamba “ni wajibu wetu wa kimaadili kuwalinda watoto wa shule zetu kutokana na hatari hii kwa uthabiti kama vile hatari za kimwili na za kiafya.”

Hatari waliyorejelea ilikuwa vitabu vilivyochukuliwa kuwa "visivyo vya Marekani, visivyo vya Kikristo, visivyo vya Kiyahudi, na visivyo vya kawaida." (Mashtaka ya chuki dhidi ya Wayahudi yalielekezwa dhidi ya riwaya kuu ya "mtengenezaji" na mwandishi wa Kiyahudi Bernard Malamud).

Mahakama, hata hivyo, iligundua, kwa mujibu wa marekebisho ya kwanza, kwamba "bodi za shule haziwezi kuondoa vitabu kutoka kwenye maktaba za shule kwa sababu tu hazipendi mawazo katika vitabu hivyo."

Riwaya ya Mmarekani Bernard Malamud (1914-1986) "The Repairman" imepewa jina la chuki dhidi ya Wayahudi na bodi za shule nchini mwake, ambao huenda hawakutambua kwamba mwandishi mwenyewe alikuwa Myahudi.

Chanzo cha picha, Getty Images

Kwa upande mwingine, udhibiti nchini Marekani una historia ndefu. Mmoja wa waathiriwa wake wa kwanza maarufu ni riwaya ya kupinga utumwa "Uncle Tom's Cabin", iliyochapishwa mnamo 1852 na Harriet Beecher Stowe.

Mnamo 1857, mtu mweusi kutoka Ohio, Sam Green, "alihukumiwa kifungo cha miaka kumi gerezani " kwa "kumiliki riwaya hiyo". Katika mabadiliko ya ajabu ya kihistoria, kitabu hiki sasa kinakosolewa zaidi na upande unaoendelea zaidi wa wigo wa kisiasa kwa taswira yake ya kijadi ya wahusika weusi.

Kadiri kitabu kinavyoangaziwa, ndivyo kinavyovutia umakini wa vidhibiti. "Heartcatcher" ya JD Salinger imekuwa ikibishaniwa mara nyingi: mwalimu alifukuzwa kazi mnamo 1960 na kitabu kiliondolewa shuleni huko Wyoming, Dakota Kaskazini na California mnamo 1980.