Messi: Simulizi ya mchezaji nguli ambaye Papa amegoma kumuita ‘Mungu’

Nyota wa Argentina Lionel Messi alitangaza Alhamisi kwamba Kombe la Dunia la 2022 nchini Qatar, lililopangwa kufanyika Novemba 20 na Disemba 18, "bila shaka" litakuwa lake la mwisho katika fainali za michuano.

"Hili ni Kombe langu la mwisho la Dunia, bila shaka," alisema nahodha wa timu ya "Tango" na mchezaji wa Paris Saint-Germain, 35, katika mahojiano na idhaa ya Argentina "ESBN".

Messi, ambaye anacheza Kombe la Dunia la nne, alicheza mechi yake ya kwanza ya kimataifa mwaka wa 2005, na kuwa mfungaji bora wa muda wote wa timu ya taifa ya Argentina akiwa na mabao 90.

Katika mahojiano na Messi mjini Paris, nyota huyo wa zamani wa Barcelona alikiri shauku yake kwa michuano hiyo mikubwa zaidi ya soka.

"Kuna wasiwasi na mvutano kuhusu Kombe la Dunia," alisema. "Hatuwezi kusubiri kwa kushiriki."

Mkataba wa Messi na Barcelona ulimalizika mwanzoni mwa Julai mwaka jana. Mnamo Agosti 10, Messi alijiunga na klabu ya Ufaransa ya Paris Saint-Germain. Alitia saini mkataba wa miaka miwili na chaguo la kuongeza mwaka mmoja zaidi.

 Jarida la Forbes linasema kuwa Messi alipata zaidi ya dola bilioni moja wakati wa taaluma yake, na ni mwanariadha wa nne kufikia hili, baada ya nguli wa gofu wa Marekani Tiger Woods, bondia wa Marekani Floyd Mayweather Jr. na nyota wa soka na mpinzani wa Ureno Cristiano Ronaldo.

Simulizi ya nguli wa soka duniani

Lionel Andres Messi Mochettini alizaliwa mnamo Juni 24, 1987 huko Rosario, Argentina. Alianza kucheza mpira wa miguu tangu utoto wake.

Mnamo 1995, alijiunga na timu ya Cubs huko Newell Old Boys (klabu ya kandanda ya daraja la kwanza iliyoko Rosario). Kulingana na Encyclopedia Britannica.

Ustadi wa ajabu wa Messi ulivutia umakini wa vilabu vya kifahari pande zote mbili za Atlantiki. Akiwa na umri wa miaka 13, alihamia Barcelona na familia yake, ambako alianza kucheza na timu ya Barcelona U-14.

Alifunga mabao 21 katika mechi 14 za timu ya vijana na haraka akajiunga na kikosi cha kwanza na kushiriki katika mechi ya kwanza isiyo rasmi. Alijiunga na Barcelona alipokuwa na umri wa miaka 16.

Msimu wa 2004-05, Messi, ambaye wakati huo alikuwa na umri wa miaka 17, alikua mchezaji mdogo na mfungaji bora zaidi kwenye La Liga.

Licha ya umbo lake la kawaida, akiwa na urefu wa mita 1.7 na uzito wa kilo 67, alikuwa na nguvu, mwenye usawaziko na mwenye uwezo mwingi uwanjani.;

Mnamo 2005 alipata uraia wa Uhispania, na mwaka uliofuata Messi na Barcelona walishinda Ligi ya Mabingwa (Mashindano ya Klabu ya Uropa).

Nyota huyo wa Argentina aliichezea timu hiyo ya Catalan michezo 778, rekodi ambayo hakuna mchezaji mwingine yeyote katika historia ya klabu hiyo ameifikia.

Messi alifunga mabao 672 akiwa na Barcelona, ​​na kushinda mataji 10 katika Ligi ya Uhispania na mataji 4 katika Ligi ya Mabingwa.

Mbali na kushinda Mpira wa Dhahabu kama mchezaji bora wa mpira wa miguu ulimwenguni mara 6.

Mara ya kwanza kwa Messi kushiriki kimataifa ilikuwa mwaka 2005 kama mchezaji wa akiba dhidi ya Hungary, alicheza kwa dakika mbili kabla ya kutolewa nje kwa kadi nyekundu, lakini haraka akathibitisha uwepo wake kwenye kikosi cha timu ya taifa na kusafiri hadi Ujerumani kushiriki fainali za kwanza za Kombe la Dunia mwaka 2006.

Alishiriki katika matoleo ya 2010 nchini Afrika Kusini, 2014 huko Brazil Wakati Argentina ilipofika fainali, na 2018 nchini Urusi.

Messi baada ya Barcelona

Mnamo 2021, Messi alitaka kutekeleza uhamisho huo wa bila malipo , lakini Barcelona walikataa, na klabu ya Catalan ilisema wakati huo kwamba yeyote anayetaka kumnunua Messi lazima alipe euro milioni 700 (pauni milioni 624). Sasa vikwazo hivyo vimepita.

Kwa muda mrefu kulikuwa na tetesi kwamba Messi angeungana tena na kocha wa zamani wa Barcelona Pep Guardiola katika klabu ya Manchester City.

Lakini pamoja na City kumsajili Jack Grealish kwa rekodi ya pauni milioni 100 nchini Uingereza, pamoja na uhamisho wa mshambuliaji wa Tottenham Harry Kane kwenda City pia kwa kiasi kikubwa, uwezekano wa Messi kuhamia klabu hiyo ya Uingereza ulipungua.

Messi aliiongoza nchi yake kuhitimisha kusubiri kwa miaka 27 kujishindia yeye na taifa lake taji la Copa America.

Gazeti la Argentina, Clarin, lilisema chini ya kichwa cha habari , "Mshtuko wa kimataifa... Je, Paris Saint-Germain itakuwa klabu yake mpya," na kubainisha kuwa klabu hiyo ya Ufaransa ndiyo "mgombea mkuu wa kutaka kuongeza nyota mwengine baada ya Kylian Mbappe na Neymar.

Gazeti hilo liliongeza, "Messi yuko kwenye kiwango cha juu cha uchezaji wake na macho yake yakiwa kwenye Kombe la Dunia huko Qatar, ataendelea kushiriki katika soka ya Ulaya," likibainisha kuwa amekuwa akitaka kujiunga na klabu ya Paris Saint-Germain, inayomilikiwa na Qatar kwa miaka mingi.

Baadhi ya timu za Argentina pia zialihitaji huduma zake, ingawa hali halisi ya kiuchumi katika mdororo wa uchumi katika nchi hii ya Marekani ya Kusini, ambayo inakabiliwa na mfumuko mkubwa wa kiuchumi, anaweza kufanya hatua yake ya kurudi nyumbani kuwa tukio la kushangaza zaidi.

Hashtag "Hello Leo" ilianza kusambaa kwenye Twitter, ambapo picha za Messi akiwa amevalia jezi za vilabu vya kifahari vya Argentina, Boca Juniors, River Plate, Newell's Old Boys na San Lorenzo, pamoja na vilabu vya kawaida zaidi kama vile Sacachipas zilisambaa.

Baada ya uvumi, Lionel Messi alijiunga na Paris Saint-Germain. Nyota huyo wa Argentina, ambaye alijiunga na klabu hiyo katika mji mkuu wa Paris kupitia uhamisho wa bila malipo , anapokea euro milioni 35 kila mwaka, na kiasi hiki hakitakuwa chini ya kodi, pamoja na motisha na vigezo vingine, kulingana na kile vyombo vya habari vya Ulaya viliripoti.

Sio Mungu

Mashabiki wa nyota huyo wa soka wa Argentina wanamwita Messi "Dios", ambalo linamaanisha "Mungu" kwa Kihispania, lakini Papa alikuwa na maoni tofauti.

Katika mahojiano na kituo cha televisheni cha Uhispania La Sexta, Papa Francis alimsifu mchezaji huyo kutoka nchini kwao Argentina, lakini akasema hatakiwi kuitwa Mungu.

Papa alisema: "Hii kwa nadharia ni kufuru. Hupaswi kufanya hivi, na watu wanaweza kumwita Mungu, kumaanisha tunakuabudu, lakini ni Mungu pekee ndiye anayestahili kuabudiwa."

Inaripotiwa kuwa Messi amemuoa mwanamitindo Antonella Roccuzzo, na wana watoto watatu, Thiago, Matteo na Sio