Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Vilabu vyamwaga mabilioni, dirisha la usajili EPL likivunja rekodi ya £3bn
Vilabu vya Ligi Kuu England vimetumia fedha nyingi kuliko wakati wowote ule kwenye dirisha moja la usajili, baada ya matumizi ya dirisha hili la kiangazi lililofungwa usiku wa jana kuvuka pauni bilioni 3.
Jumla ya pauni bilioni 2.73 zilikuwa zimetumika hadi kufikia tarehe 31 Agosti, lakini usajili wa dakika za mwisho ukiongozwa na usajili wa Alexander Isak kutoka Newcastle kwenda Liverpool kwa ada ya rekodi ya Uingereza ya pauni milioni 125, zimefanya jumla ya matumizi kufikia pauni bilioni 3.087.
Matumizi haya ni makubwa zaidi ikilinganishwa na dirisha la kiangazi lililopita, ambapo vilabu vya ligi kuu vilitumia pauni bilioni 1.96 pekee.
Kiwango cha matumizi katika dirisha hili pia ni kikukubwa zaidi kuliko matumizi yote ya usajili katika ligi ya ujerumani (Bundesliga), Hispania (La Liga), Ufaransa (Ligue 1) na Italia (Serie A).
Nani alimmwaga pesa zaidi?
Liverpool wamevunja rekodi ya usajili katika dirisha hili kiangazi. Kikosi cha kocha Arne Slot kimemsajili Isak na kupelekea matumizi yao ya usajili kwa dirisha hili tu la kiangazi kufikia pauni milioni 415 na kuweka rekodi mpya ya kiasi kikubwa zaidi kutumika na klabu moja kwenye dirisha moja la usajili.
Rekodi ya awali ilikuwa ya Chelsea, waliotumia pauni milioni 400 katika dirisha la usajili la kiangazi mwaka 2023.
Hii si tu kwamba ni zaidi ya klabu yoyote ya Ulaya, bali karibu sawa na jumla ya matumizi ya ligi zingine zote za Ulaya.
"Liverpool imeonyesha nguvu kubwa," alisema kipa wa zamani wa Manchester City Joe Hart.
"Usajili na pesa walizotumia ni za ajabu, na wamewaleta baadhi ya wachezaji bora kabisa."
Chelsea na Arsenal pia walifanya usajili mkubwa ili kuimarisha vikosi vyao na kupambana zaidi kwa ubingwa, ambapo Chelsea walitumia pauni milioni 285 na Arsenal milioni 255 mtawalia.
Lakini Chelsea pia walifanikiwa kuuza wachezaji kukusanya pauni milioni 288 kutokana na mauzo na kujipatia faida ya pauni milioni 3, huku Arsenal wakifanikiwa kupata pauni milioni 9 pekee kutokana na mauzo ya wachezaji wake, na hivyo kutumia jumla ya pauni milioni 246.
Nani kaenda wapi siku ya mwisho ya usajili Ulaya?
Dirisha la uhamisho wa majira ya joto - limefungwa Jumatatu, Septemba 1 kwa vilabu vya Ligi Kuu ya England. Mbali na kuvunja rekodi ya matumizi limeshuhudia pia nyota kadhaa wakishindwa kuhama timu zao kwa sababu mbalimbali.
Aston Villa hawakupokea ofa kutoka Manchester United kwa ajili ya kipa wa Argentina Emiliano Martinez licha ya mchezaji huyo mwenye miaka 32 kuhusishwa sana na uhamisho wa kuelekea Old Trafford.
Liverpool walikataa kumruhusu Joe Gomez, 28, kujiunga na AC Milan baada ya mpango wao wa kumsajili beki wa England Marc Guehi, 25, kutoka Crystal Palace kuvunjika.
Waliosajiliwa Ligi Kuu England
Reiss Nelson [kutoka Arsenal - kwenda Brentford] kwa mkopo
Oleksandr Zinchenko [kutoka Arsenal - kwenda Nottingham Forest] mkopo
Igor Julio [kutoka Brighton – kwenda West Ham United] kwa mkopo
Dilane Bakwa [kutoka Strasbourg – kwenda Nottingham Forest]
Bertrand Traore [kutoka Ajax – kwenda Sunderland]
Harvey Elliott kutoka [Liverpool – kwenda Aston Villa] kwa mkopo
Senne Lammens [kutoka Royal Antwerp – kwenda Manchester United] £18.1 milioni
Yoane Wissa [kutoka Brentford – kwenda Newcastle] £55 milioni
Kevin [kutoka Shakhtar – kwenda Fulham] £34.6 milioni
Brian Brobbey [kutoka Ajax - kwenda Sunderland] £21.6 milioni
Jadon Sancho [kutoka Manchester United – kwenda Aston Villa] mkopo
Alexander Isak [kutoka Newcastle - kwenda Liverpool] £125 milioni
Merlin Rohl [kutoka Freiburg – kwenda Everton] kwa mkopo
Cuiabano [kutoka Botafogo – kwenda Nottingham Forest]
Samuel Chukwueze [kutoka AC Milan - kwenda Fulham] kwa mkopo
Randal Kolo Muani [kutoka PSG – kwenda Tottenham] kwa mkopo
Piero Hincapie [kutoka Bayer Leverkusen – kwenda Arsenal] mkopo
Lutsharel Geertruida [kutoka RB Leipzig – kwenda Sunderland] mkopo
Jaydee Canvot [kutoka Toulouse – kwenda Crystal Palace]
Veljko Milosavljevic [kutoka Red Star Belgrade – kwenda Bournemouth] £13 milioni
Tolu Arokodare [kutoka Genk – kwenda Wolves] £24 milioni
Facundo Buonanotte [kutoka Brighton – kwenda Chelsea] kwa mkopo
Victor Lindelof [kutoka Manchester United – kwenda Aston Villa] bure
Alex Jimenez [kutoka AC Milan – kwenda Bournemouth] kwa mkopo
Waliokwenda kimataifa kutoka England
Jamie Vardy [kutoka Unattached – kwenda Cremonese] bure
Nicolas Jackson [kutoka Chelsea – kwenda Bayern Munich] kwa mkopo
Cyriel Dessers [kutoka Rangers – kwenda Panathinaikos]
Abu Kamara [kutoka Hull – kwenda Getafe] kwa mkopo
Jakub Kiwor [kutoka Arsenal – kwenda Porto] kwa mkopo
Fabio Vieira [kutoka Arsenal – kwenda Hamburg] kwa mkopo
Musa Drammeh [kutoka Heart of Midlothian – kwenda Torreense]
Ben Chilwell [kutoka Chelsea -kwenda Strasbourg]
Antony [kutoka Man Utd – kwenda Real Betis] £21.65 milioni
Odsonne Edouard [kutoka Crystal Palace – kwenda Lens]
Rasmus Hojlund [kutoka Man Utd – kwenda Napoli] kwa mkopo
Jeremy Sarmiento [kutoka Brighton – kwenda Cremonese] kwa mkopo
Darko Churlinov [kutoka Burnley – kwenda Kocaelispor]
Martial Godo [kutoka Fulham - kwenda Strasbourg]
Eric da Silva Moreira [kutoka Nottingham Forest – kwenda Rio Ave] kwa mkopo
Emerson Palmieri [kutoka West Ham – kwenda Marseille]
Sambi Lokonga [kutoka Arsenal – kwenda Hamburg]
Bilal El Khannouss [kutoka Leicester – kwenda Stuttgart] kwa mkopo
Norman Bassette [kutoka Coventry - kwenda Reims] kwa mkopo
Oscar Cortes [kutoka Rangers – kwenda Sporting Gijon] kwa mkopo
Abdoulaye Kamara [kutoka Portsmouth – kwenda FC Saarbrucken] bure
Tariq Lamptey [kutoka Brighton – kwenda Fiorentina]
Szabi Schon [kutoka Bolton – kwenda ETO Gyor] kwa mkopo.