Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ndege zaonywa kutosafiri katika anga ya Bali baada ya Volkano kulipuka
Kampuni za ndege zimeonywa kuhusu hatari ya jivu la volkano angani kariibu na kisiwa cha Indonesia Bali baada ya mlima wa volcano kulipuka na kusababisha kutanda kwa moshi mweusi mwingi katika urefu wa mita mia moja na kumi na tano angani.
Onyo hilo kwa sekta ya ndege inataja masalio ya volkano yaliotanda angani juu ya mlima Agung katika kisiwa hicho cha Bali.
Maafisa huko wanasema wana wasiwasi huenda mlima huwa ukalipuka kikamilifu hatua itakayo kuwa inashuhudiwa kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1963, wakati takriban watu 1600 walipouawa.
Ni tukio la pili la kuplipuka mlima wa volkano katika wiki, na watu wanaoishi kwa umbali wa kilomita nane kutoka mlima huo wameagizwa kuyahama makaazi yao.
Bali ni kivutio kikuu cha utalii.
Uwanja wake mkuu wa ndege unafanya kazi kama kawaida, licha ya kwamba baadhi ya kampuni za ndege zimesitisha safari tangu kuanza kuchemka kwa mlima mnamo September.