Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Brazil: Rais Lula kuchunguzwa kwa tuhuma za ufisadi
Mahakama kuu nchini Brazil imesema kuwa Rais wa zamani wa nchi hiyo Luiz Inácio Lula da Silva atachunguzwa ili kuthibitisha kama kweli alihusika katika kashfa ya ufisadi kwenye kampuni kubwa ya mafuta nchini humo Petrobras.
Waendesha mashitaka nchini humo wamesema kuwa Lula alikuwa muhimili mkubwa katika utekelezwaji wa rushwa hiyo.
Lula amekana kuhusika na kusema kuwa hizo ni mbinu za kisiasa za kumzuia kuwania urais mwaka 2018.