Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Roboti yafanya upasuaji wa macho mara ya kwanza duniani
Madaktari wametumia roboti ya kwanza kufanya upasuaji wa macho na kurejesha uwezo wa kuona kwa mgonjwa kwa mara ya kwanza duniani.
Kundi la madaktari kutoka hospitalia ya John Radclife nchini Uingereza, walitumia roboti hiyo kutoa ngozi nyembamba zaidia kutoka jicho la mgonjwa.
Mgonjwa kwa jina Bill Beaver mwenye umri wa miaka 70 aliyefanyiwa upasuaji huo sasa anasema anahisi vyema.
Madaktari wana matumaini kuwa mfumo huo utasaidia katika upasuaji unaohitaji umakini zaidi.