Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ugonjwa wa polio bado tishio nchini Nigeria
Nigeria imeripoti kesi mbili za ugonjwa wa polio katika jimbo la Borno eneo ambalo kuna idadi kubwa ya wapiganaji wa Boko Haram.Watoto wawili wamepooza kutokana na ugonjwa huo.
Shirika la afya duniani limesema ndio kesi za kwanza kwa miaka miwili sasa.
Kesi hizi zimekwamisha matumaini ya kukomesha Polio kwa mwaka huu.
Umoja wa mataifa umekanusha uvumi kuwa chanjo za polio zina lengo la kusababisha kutozaa kwa wailsamu