Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Makamu rais wa zamani wa FIFA ahukumiwa kifungo cha miaka tisa gerezani
Makamu Rais wa zamani wa FIFA amehukumiwa kifungo cha miaka tisa gerezani nchini Marekani ikiwa ni matokeo ya uchunguzi wa ruhswa iliyofanywa ndani ya chombo hicho kikubwa cha soka duniani.
Juan Angel Napout, ambaye anatokea Paraguay alipatikana na hatia ya kuchukua mamilioni ya dola kwa njia ya rushwa.
Hatua hii inakuja siku chache baada ya kifungo cha miaka minne alichopewa mkuu wa zamani wa soka Brazil Jose Maria Marin ambaye pia alihusishwa kwenye tuhuma hizohizo.
Wote kwa pamoja walikutwa na hatia ya kupokea rushwa kutoka kwa makampuni makubwa ambayo yalikua yakijitangaza kupitia FIFA.