Messi: Inaniuma sana kukosa penalti Kombe la Dunia

Lionel Messi alimefunga jumla ya magoli 48 katika msimu wa mwaka 2017/2018

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Lionel Messi alimefunga jumla ya magoli 48 katika msimu wa mwaka 2017/2018

Lionel Messi amesema inamuumiza sana baada ya Penati yake dhidi ya Iceland kuokolewa wakati Argentina ilipokutana na Iceland.

Mkwaju wa penati wa Mchezaji huyu,30 na nyota wa Barcelona haukuleta madhara mbele ya mlinda mlango Hannes Halldorsson na kufanya timu hizi mbili kutoka sare ya 1-1

Messi alikuwa na matumaini makubwa ya kufanya vyema akitazama matokeo ya hasimu wake wa siku nyingi Cristiano Ronaldo hasa mabao matatu aliyoyafunga siku ya ijumaa dhidi ya Uhispania.

''Tumepata uchungu kwa kukosa alama tatu, kuanza kwa ushindi ni muhimu sana wakati wote, sasa tunapaswa kufikiria kuhusu Croatia''.

''tutajitahidi kuhakikisha hili linapita haraka''.

Messi alisema mbinu ya Iceland ilifanya mchezo ukawa mgumu ''hawakutaka kucheza'' lakini alikiri kuwa walijihami kwa ''kiasi kikubwa''

Messi akipiga Penati katika mchezo ambao uliishia kwa sare ya 1-1 kati ya Iceland na Argentina

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Messi akipiga Penati katika mchezo ambao uliishia kwa sare ya 1-1 kati ya Iceland na Argentina

Kocha wa Argentina Jorge Sampaoli alimsifu Messi namna alivyocheza katika mchezo huu mgumu

''kutathimini kazi aliyoifanya Messi ni ngumu kwa sababu haikuwa mechi nzuri kwake''.

''Iceland walicheza kwa kujihami sana, wakifunga nafasi zote lakini tulifanya kila tuwezalo ili kushinda.Leo anajitoa kwa Argentina''.

''Mara zote huwa trunakuja kushinda, ndio maana kumekuwa na hali ya taharuki''.

Argentina itakabiliana na Croatia siku ya Alhamisi katika uwanja wa Nizhny Novgorod.

Mlinda mlango wa Iceland Hannes Halldorsson alikuwa mchezaji nyota wa mchezo huo

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mlinda mlango wa Iceland Hannes Halldorsson alikuwa mchezaji nyota wa mchezo huo

Mlinda mlango wa Iceland Hannes Halldorsson ameeleza jitihada alizofanya kuhakikisha anapangua mipira ya Messi.

Anasema alitazama penati nyingi za Messi na kutafuta mbinu ya kuzikabili.

''Ni ndoto iliyotimia kuishinda penati, hasa kwa kuwa imetusaidia kupata alama moja ambayo ni muhimu katika kufuzu hatua ya makundi''.