Iceland walivyomzima Messi - kwa picha

Muda wa kusoma: Dakika 3

Iceland mwanzoni mwa Kombe la Dunia walikuwa wametazamwa kama wanyonge ambao wangekabiliwa na maangamizi dhidi ya 'masihi' Lionel Messi.

Wengi walitarajia taifa hilo na watu 335,000 pekee lifungwe mabao mengi sana Jumamosi. Lakini walibadilisha hilo na badala yake wakatoka sare na Argentina.

messi

Chanzo cha picha, AFP/Getty

Hapa ni yalivyotokea kwa picha.

Iceland fans thunder clap in Moscow

Chanzo cha picha, Reuters

Kabla ya mechi kuanza, mashabiki wa Iceland walipiga makofi kwa pamoja, kama kawaida yao.

Taifa lao lina watu 335,000 pekee, iwapo mashabiki walioonekana Moscow ni raia wa taifa hilo, basi ni kama taifa lote lilikuwa limesafiri.

Argentine fan with Messi picture

Chanzo cha picha, AFP/Getty

Mashabiki wa Argentina walijaribu kuwanyamazisha, kwa bango na kumrejelea nyota wao anayechezea Barcelona Lionel Messi.

Je, angeweza kufikia kiwango kilichofikiwa na mshindani wake mkuu Cristiano Ronaldo siku iliyotanguliwa?

Angefanikiwa?

Ruka X ujumbe, 1
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 1

Presentational white space
Aguero celebrates

Chanzo cha picha, EPA

Argentina walifunga kwanza kupitia Sergio Aguero na wengi wakatarajia kichapo kikali kwa Iceland.

Iceland score

Chanzo cha picha, Reuters

Finnbogason celebrates

Chanzo cha picha, Reuters

Lakini Iceland walikomboa kupitia Alfred Finnbogason, na kuzua shangwe na nderemo uwanjani.

Macho yote sasa yakaelekezwa kwa Messi, angefanikiwa kuupenya ukuta wa Iceland?

Messi misses penalty

Chanzo cha picha, Reuters

Messi misses penalty

Chanzo cha picha, Reuters

Ronaldo alikuwa amefunga penalti, lakini Messi alipopata fursakama hiyo, ilizuiwa na kipa Hannes Halldorsson.

Isitoshe, alishindwa kufunga frikiki dakika za mwisho tofauti na Mreno Ronaldo ambaye alikuwa amefunga kwa mpira kumponyoka kipa wa Uhispania David de Gea kwa bao lake la pili. Kombora la Messi lilielekea nje ya goli la Iceland.

Messi

Chanzo cha picha, Reuters

Messi after the match

Chanzo cha picha, Reuters

Haikuwa siku nzuri kwa Messi.

Maradona reacts

Chanzo cha picha, Reuters

Kwa timu ya taifa, messi angalau amebaki kuwa chini ya shujaa mwingine Diego Maradona ambaye alikuwa akiitazama mechi hiyo.

Maradona alieleza kusikitishwa kwake na uchezaji wa taifa hilo Urusi.

Ruka X ujumbe, 2
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 2

Presentational white space

Wakati huu, wengi katika mitandao ya kijamii, Maradona ambaye hufahamika sana kwa bao lake la 'mkono wa Mungu' alionekana akiwa ameshika sigara akitazama Messi uwanjani, kinyume na sheria za Fifa kwamba uvutaji wa sigara hauruhusiwi uwanjani.

Iceland goalkeeper Hannes Halldorsson

Chanzo cha picha, EPA

Badala yake, ilikuwa ni siku ya kipa Halldorsson ambaye ustadi wake ulisaidia Iceland kujimudu dhidi ya Argentina.

Jubilation in Reykjavik after the match ended

Chanzo cha picha, AFP/Getty

Mji mkuu wa Iceland Reykjavik kulijaa shangwe baada ya kipenga cha mwisho kupulizwa, licha ya mvua kubwa kunyesha.

Argentine fan

Chanzo cha picha, Reuters

Mashabiki wa Argentina hata hivyo walijawa na masikitiko, masihi wao Messi alikuwa ameshindwa kuvuma. Wangelazimika kusubiri wakati mwingine.

Unaweza kusoma pia:

Presentational white space

Picha zote zina hakimiliki