Iceland walivyomzima Messi - kwa picha
Iceland mwanzoni mwa Kombe la Dunia walikuwa wametazamwa kama wanyonge ambao wangekabiliwa na maangamizi dhidi ya 'masihi' Lionel Messi.
Wengi walitarajia taifa hilo na watu 335,000 pekee lifungwe mabao mengi sana Jumamosi. Lakini walibadilisha hilo na badala yake wakatoka sare na Argentina.

Chanzo cha picha, AFP/Getty
Hapa ni yalivyotokea kwa picha.

Chanzo cha picha, Reuters
Kabla ya mechi kuanza, mashabiki wa Iceland walipiga makofi kwa pamoja, kama kawaida yao.
Taifa lao lina watu 335,000 pekee, iwapo mashabiki walioonekana Moscow ni raia wa taifa hilo, basi ni kama taifa lote lilikuwa limesafiri.

Chanzo cha picha, AFP/Getty
Mashabiki wa Argentina walijaribu kuwanyamazisha, kwa bango na kumrejelea nyota wao anayechezea Barcelona Lionel Messi.
Je, angeweza kufikia kiwango kilichofikiwa na mshindani wake mkuu Cristiano Ronaldo siku iliyotanguliwa?
Angefanikiwa?
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 1


Chanzo cha picha, EPA
Argentina walifunga kwanza kupitia Sergio Aguero na wengi wakatarajia kichapo kikali kwa Iceland.

Chanzo cha picha, Reuters

Chanzo cha picha, Reuters
Lakini Iceland walikomboa kupitia Alfred Finnbogason, na kuzua shangwe na nderemo uwanjani.
Macho yote sasa yakaelekezwa kwa Messi, angefanikiwa kuupenya ukuta wa Iceland?

Chanzo cha picha, Reuters

Chanzo cha picha, Reuters
Ronaldo alikuwa amefunga penalti, lakini Messi alipopata fursakama hiyo, ilizuiwa na kipa Hannes Halldorsson.
Isitoshe, alishindwa kufunga frikiki dakika za mwisho tofauti na Mreno Ronaldo ambaye alikuwa amefunga kwa mpira kumponyoka kipa wa Uhispania David de Gea kwa bao lake la pili. Kombora la Messi lilielekea nje ya goli la Iceland.

Chanzo cha picha, Reuters

Chanzo cha picha, Reuters
Haikuwa siku nzuri kwa Messi.

Chanzo cha picha, Reuters
Kwa timu ya taifa, messi angalau amebaki kuwa chini ya shujaa mwingine Diego Maradona ambaye alikuwa akiitazama mechi hiyo.
Maradona alieleza kusikitishwa kwake na uchezaji wa taifa hilo Urusi.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 2

Wakati huu, wengi katika mitandao ya kijamii, Maradona ambaye hufahamika sana kwa bao lake la 'mkono wa Mungu' alionekana akiwa ameshika sigara akitazama Messi uwanjani, kinyume na sheria za Fifa kwamba uvutaji wa sigara hauruhusiwi uwanjani.

Chanzo cha picha, EPA
Badala yake, ilikuwa ni siku ya kipa Halldorsson ambaye ustadi wake ulisaidia Iceland kujimudu dhidi ya Argentina.

Chanzo cha picha, AFP/Getty
Mji mkuu wa Iceland Reykjavik kulijaa shangwe baada ya kipenga cha mwisho kupulizwa, licha ya mvua kubwa kunyesha.

Chanzo cha picha, Reuters
Mashabiki wa Argentina hata hivyo walijawa na masikitiko, masihi wao Messi alikuwa ameshindwa kuvuma. Wangelazimika kusubiri wakati mwingine.
Unaweza kusoma pia:

Picha zote zina hakimiliki












