India yafanyia majaribio kombora jipya lenye uwezo wa kurusha makombora mengi kwa wakati mmoja

Chanzo cha picha, Hindustan Times via Getty
Jeshi la India limefanyia majaribio kizazi kipya cha makombora ya hali ya juu ya Agni kwenye pwani ya Odisha.
Kombora hili linaweza kurusha makombora mengi katika maeneo tofauti.
Kulingana na Wizara ya Ulinzi ya India, mfumo huu wa makombora ulijaribiwa mnamo Ijumaa, Mei 8.
"India mnamo Mei 8 ilifanikiwa kujaribu kombora la hali ya juu la Agni lenye mfumo wa MIRV kutoka Kisiwa cha Abdul Kalam, Odisha," Wizara ya Ulinzi ilisema katika taarifa.
Taarifa hiyo iliendelea kwa kusema kuwa kombora hilo lenye vichwa vingi vya kivita, lililenga maeneo kadhaa yaliyotengwa katika eneo pana la kijiografia katika Bahari ya Hindi.
Uzalishaji wa makombora ya Agni ulianza nchini India mwaka 1983. Kizazi kilichopita (cha tano) Agni ni balestiki nunayoweza kusafiri kutoka bara moja hadi jingine pamoja na kuwa na uwezo wa kubeba kichwa cha nyuklia, mbali na kwamba kombora hilo linaweza kusafiri umbali wa kilomita 5,000.




