Meneja wa zamani wa Man City Manuel Pellegrini aporwa na majambazi wenye bunduki

Manuel Pellegrini

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Pellegrini amewashukuru polisi wa Chile kwa ujasiri wao na kwa kufika eneo la tukio upesi sana.
Muda wa kusoma: Dakika 1

Meneja wa West Ham Manuel Pellegrini ameporwa na majambazi waliokuwa na bunduki nchini Chile.

Mkufunzi huyo maarufu sana duniani ambaye aliwahi kuwa meneja wa mabingwa wa England Manchester City alikuwa njiani kuelekea kwenye mgahawa mmoja mjini mkuu wa Chile, Santiago, akiwa na mke na marafiki wawili pale walipovamiwa.

Msemaji wa West Ham United amesema: "Tuna furaha kusikia kwamba Manuel na mkewe wako salama, hawakudhuriwa."

Kupitia ujumbe wa Twitter aliouandika kwa Kihispania, Pellegrini amewashukuru polisi wa Chile kwa ujasiri wao na kwa kufika eneo la tukio upesi sana.

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe

Pellegrini, ambaye ni mzaliwa wa Chile, aliteuliwa meneja wa West Ham mwezi Mei.

Mwenyekiti mwenza wa klabu hiyo David Sullivan amesema amewasiliana naye kuma ujumbe wa heri na kumpa pole.

Gazeti la Chile La Cuarta limesema kipochi cha mke wa pellegrini kimeibiwa.

Afisa mmoja wa serikali ameambia gazeti hilo kwamba genge hilo la majambazi liliwafyatulia polisi risasi kabla ya kutoroka kwa kuutmia gari aina ya Porsche ambalo walikuwa wameliiba.

Meneja huyo wa zamani wa Manchester City na Real Madrid aliacha kazi klabu ya Hebei China Fortune ya China mwezi jana.

Alishinda Liig ya Premia akiwa na City mwaka 2014.