Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Manchester City yaikung'uta Arsenal 3-1
Manchester City waliwakung'uta Arsenal 3-1 na kufungua mwanya wa pointi kileleni mwa ligi ya Premier.
Bao la Kevin de Bruyne na penalti ya Sergio Aguero iliiweka Man City katika nafasi ya kushinda ligi ya tisa.
Licha ya Alexandre Lacazette kuipa Arsenal bao la kuvuta machozi, Gabriel Jesus aliipa Manchester ushindi kwa kuifungia bao la tatu.
Arsenal huenda wangepata kipigo zaidi isingekuwa ni jitihada za kipa Petr Cech
Mafanikio ya Manchester City dhidi ya Machester United walio nafasi ya pili yatatokana na matokeo ya leo dhidi ya Chelsea.