Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Messi awika, Barcelona yaizaba Juventus 3-0
Mabao mawili ya Lionel Messi yalitosha kuisaidia Barcelona kuiadhibu Juventus mabao 3-0 katika uwanja wa Nou Camp.
Messi alifunga bao la kwanza baada ya kupa ni kupe na mshambuliaji Luis Suarez.
Ivan Rakitic aliifungia Barcelona bao la pili baada ya shambulio la Messi kuokolewa katika laini ya goli.
Mshambuliaji huyo wa Argentina baadaye alihakikisha kuwa timu yake inachukua ushindi dhidi ya Juventus walioshiriki katika fainali ya kombe hilo mwaka uliopita baada ya kufunga bao zuri kwa kutumia mguu wake wa kushoto kwa umbali wa maguu 20.
Akicheza mbele ya mabeki wa Juve, Messi aliwachenga mabeki waliokuwa wakimkaba kabla ya kumwacha kipa wa miaka mingi Gianluigi Buffon bila jibu.