Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Florentin Pogba kukabiliana na nduguye Paul Pogba
Mchezaji wa kimataifa wa Guinea Florentin Pogba amekiri kuwa mamake atakuwa katika hali ngumu wakati atakapotazama akimkabili nduguye mdogo Paul katika mechi ya ligi ya Europa.
Siku ya Alhamisi Florentin ataichezea St Etienne dhidi ya Paul Pogba anayechezea Manchester United.
''Haitakuwa rahisi kwake lakini ni wakati muhimu kuwaona wanawe wakicheza'' ,alisema beki huyo.
''Pengine matokeo mazuri kwake itakuwa sare, lakini sote wawili tutajitolea kuona kwamba tunapata matokeo mazuri kwa timu zetu. Yeyote atakayeibuka mshindi atafurahia''.
Mechi ya siku ya Alhamisi itakuwa ya kwanza kwa ndugu hao wawili waliokulia karibu na mji mkuu wa Ufaransa Paris, watapambana katika uwanja wa soka.