Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Real Madrid wafikia rekodi ya Barca La Liga
Real Madrid wamecharaza Espanyol 2-0 na kufikia rekodi ya Barcelona ya kushinda mechi 16 mfululizo katika ligi kuu ya Uhispania, La Liga.
Ushindi wao mechi hiyo ya Jumapili umewaweka alama tatu mbele kileleni mwa ligi hiyo.
Mabao kutoka kwa James Rodriguez na Karim Benzema yaliwawezesha kufikia rekodi hiyo iliyowekwa na Barcelona walipokuwa chini ya Pep Guardiola msimu wa 2010-11.
Real, walicheza bila nyota wao Gareth Bale na Cristiano Ronaldo ugenini uwanja wa Cornella-El Prat lakini hilo halikuwazuia kuandikisha ushindi wao wa nne kutoka kwa mechi nne walizocheza msimu huu.
Barcelona wanashikilia nafasi ya pili ligini kwa sasa wakiwa na alama tisa, sawa na Las Palmas. Madrid wana alama 12.