Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kupiga
kura baadaye leo kuhusu rasimu za maazimio kuhusu vita nchini Iran na athari
zake katika eneo hilo.
Azimio la kwanza - lililotolewa na nchi za Ghuba - inalaani
mashambulizi dhidi yao na Jordan na Iran.
Urusi - mshirika wa Iran katika baraza hilo - imeanzisha
rasimu nyingine. Bila kutaja Iran, Israel au Marekani, inalaani mashambulizi
yote dhidi ya raia na yanawasihi pande zote kuacha kupigana na kurudi kwenye meza
ya mazungumzo.
Ni hatua ya kwanza kuzingatiwa na baraza tangu lilipofanya
mkutano wa dharura muda mfupi baada ya mzozo kuzuka.
Akihutubia wanachama wakati huo, Katibu Mkuu wa Umoja wa
Mataifa Antonio Guterres alisema mashambulizi ya anga kati ya Israel na
Marekani dhidi ya Iran, na mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Iran dhidi ya
nchi katika eneo hilo yalikuwa ukiukaji wa katiba ya Umoja wa Mataifa.
Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa Amir Saeid Iravani
alikosoa nchi za Ghuba - akizishutumu kwa kujaribu kubadilisha majukumu ya
mchokozi na mwathiriwa kupitia kile alichokiita upendeleo wenye msukumo wa
kisiasa.
Rasimu hiyo sasa ina wadhamini zaidi ya 90 - ikiwa ni pamoja
na Uingereza. Inataka kusitishwa mara moja kwa mashambulizi na vitisho vyote
kutoka Iran dhidi ya nchi sita za Ghuba na Jordan, ikiwa ni pamoja na kupitia
washirika.
Pia inalaani vitendo au vitisho vyovyote kutoka Tehran
ambavyo vitafunga au kuingilia urambazaji wa kimataifa kupitia Mlango-Bahari
muhimu wa Hormuz.
Iran yaanzisha wimbi jipya la mashambulizi
Katika saa chache zilizopita, Iran imezindua wimbi jipya la
mashambulizi dhidi ya maeneo lengwa ya Israel na Marekani Mashariki ya Kati.
Vyombo vya habari vya serikali ya Iran vilisema ghasia hizo
zilikuwa "kali zaidi na nzito zaidi" tangu kuanza kwa mzozo huo, AFP
iliripoti.
Israeli inasema ilitambua makombora yaliyorushwa kutoka
Iran, ingawa baadaye iliongeza kuwa ilikuwa salama kwa raia kuondoka katika
makazi.
Saudi Arabia ilisema kwamba ilikuwa imezuia na kuharibu
ndege mbili zisizo na rubani zilizokuwa zikielekea kwenye eneo la mafuta.
Ving'ora pia vilisikika nchini Bahrain, ambayo ndiyo
makao makuu ya Kikosi cha Tano cha Jeshi la Wanamaji la Marekani.