Putin aweka masharti magumu kusitishaji mapigano
Taarifa kutoka Ikulu ya Marekani kuhusu mazungumzo ya Trump na Putin inaonyesha kuwa amekataa ombi la kusitisha mapigano haraka ya ardhini, angani na baharini, badala yake, Putin amekubali kusimamisha mashambulizi ya makombora ya masafa marefu kwenye miundombinu ya nishati ya Ukraine.
Hili lilikuwa pendekezo la Ukraine ambalo Wamarekani walilipuuza wiki moja iliyopita.
Trump na Putin pia wameonekana kukubaliana kufanya mazungumzo ya haraka kupata suluhu ya muda mrefu.
Vladmir Putin amemthibitishia Trump "ahadi yake ya msingi" ya makubaliano ya azimio la amani lakini kwa masharti yafuatayo:
- Taarifa ya Urusi inasema Putin alimwambia Trump "sharti muhimu" la kuzuia kuongezeka kwa mzozo "linapaswa kuwa kukomesha kabisa misaada ya kijeshi ya kigeni na kushirikishana taarifa za kijasusi na Ukraine"
- Putin pia alizungumzia kuhusu "hitaji la kukomesha usajili wa wanajeshi wa kulazimishwa nchini Ukraine na upangaji upya wa Vikosi vya Wanajeshi wa Ukraine"
- Makubaliano yoyote "yanapaswa kuwa magumu, thabiti na ya muda mrefu" na lazima "yazingatie hitaji kamili la kuondoa sababu kuu za mgogoro", taarifa hiyo ilisema.
- Pia lazima izingatie "maslahi halali ya Urusi katika eneo la usalama"