Mauzo ya China yaongezeka licha ya ushuru wa Trump
Mauzo ya bidhaa za China nje ya nchi yaliongezeka katika miezi miwili ya kwanza ya mwaka huu licha ya mgogoro wa kibiashara kati ya taifa hilo na Marekani.
Takwimu rasmi zinaonyesha kwamba bidhaa zinazotumwa nje ya nchi ziliongezeka kwa asilimia 20 mwezi Januari na Februari. Hii ni zaidi ya mara tatu ya makadirio ya wanauchumi.
Ongezeko hili linaiweka taifa hilo katika nafasi nzuri ya kuvunja rekodi yake iliyoweka mwaka 2025 ambapo kiwango cha bidhaa zilizouzwa nje ya nchi kilipita kiwango cha bidhaa zilizoagizwa kuingia nchini humo.
Tangazo hilo linakuja huku Rais wa Marekani Donald Trump akitarajiwa kuzuru China mapema mwezi Aprili kukutana na mwenzake wa China Xi Jinping.
Uchumi wa China ambao ni wa pili kwa ukubwa duniani unategemea sana mauzo ya nje huku ikikabiliwa na masuala kadhaa ikiwa ni pamoja na matumizi duni ya walaji, kupungua kwa idadi ya watu na mgogoro wa soko la bidhaa.
Soma pia: