Iran yawasilisha pendekezo jipya la mazungumzo kwa Marekani
Tehran imewasilisha pendekezo jipya la mazungumzo na Marekani kupitia mpatanishi, Pakistan, shirika la habari la serikali ya Iran (IRNA) limeripoti.
Hii imeonekana kama hatua ya kujaribu kumaliza mvutano uliopo kati ya Marekani na Iran.
Shirika la habari la IRNA halijatoa maelezo Zaidi kuhusu pendekezo hilo, lakini bei za mafuta duniani, ambayo ilikuwa imepanda maradufu, imeshuka baada ya Iran kuwasilisha pendekezo hilo.
“Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imewasilisha mapendekezo yake ya hivi karibuni kwa Pakistan, kama mpatanishi katika mazungumzo na Marekani, usiku wa Alhamisi,” Shirika la habari la IRNA limeandika.
Baada ya makubaliano ya kusitisha mapigano kuanza kutekelezwa tarehe 8 mwezi Aprili, Islamabad iliandaa mazungumzo kati ya wajumbe wa Tehran na Washington, ikilenga kuafikia makubaliano ya kumaliza vita vilivyoanza baada ya shambulio la Marekani na Israel dhidi ya Iran tarehe 28 mwezi Februari.
Mazungumzo hayo yalitibuka bila maafikiano yoyote.
Pia unaweza kusoma: