"Kiongozi mkuu wa Iran yuko salama" - Iran

Chanzo cha picha, Getty Images
Ayatollah Mohsen Qomi, ambaye ni mwanachama wa baraza la wataalamu , na pia anahudumu katika ofisi ya kiongozi mkuu wa Iran, amepuuzia madai yanayotilia shaka afya ya kiongozi mkuu wa taifa hilo, Mojtaba Khamenei.
Qomi amesema kiongozi huyo yuko salama, na anaendelea na majukumu yake ya kitaifa, na kudai kuwa uvumi unaoenezwa unatoka kwa mataifa ya magharibi.
“Baadhi ya watu wanauliza kuhusu hali ya afya ya Kiongozi wetu mtukufu, Ayatollah Sayyid Mojtaba Khamenei.Ni maadui wanaouliza, ‘Kwa nini haonekani hadharani? Kwa nini hatumi ujumbe wa sauti au video? Kwa nini waliomtembelea hawazungumzi?’ Wanataka kutumia maswali haya kutulazimisha kujibu ili wafanikishe malengo yao,” aliliambia shirika la habari la Fars News Agency
Qomi aliongeza kuwa licha ya majeraha aliyopata, viongozi wa Iran kwa sasa wanaangazia kwa umakini kulinda maisha ya kiongozi huyo.
“Kwa sasa, jambo muhimu zaidi ni kuhakikisha tunahifadhi maisha ya Kiongozi wetu, licha ya majeraha aliyoyapata, Mwenyezi Mungu amemhifadhi” alisema Qomi.
Pia unaweza kusoma:










