Wanajeshi wa Ulaya wawasili Greenland, Trump asema Marekani inakihitaji kisiwa hicho

Chanzo cha picha, AFP via Getty Image
Kikosi cha wanajeshi 15 wa Ufaransa kimewasili katika mji mkuu wa Greenland Nuuk, huku mataifa kadhaa ya Ulaya yakituma wanajeshi huko kama sehemu ya kile kinachoitwa ujumbe wa upelelezi.
Hatua hiyo, ambayo pia itajumuisha kupelekwa Greenland kwa wanajeshi kutoka mataifa ya Ujerumani, Uswidi, Norway, Uholanzi na Uingereza, inakuja wakati Rais wa Marekani, Donald Trump kuendelea na mpango wake wa kutaka kukimiliki kisiwa hicho cha Arctic, ambacho ni sehemu inayojitegemea ya Denmark.
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema kikosi cha kwanza kitaimarishwa hivi karibuni na "mali ya ardhini, angani na baharini".
Mwanadiplomasia mkuu Olivier Poivre d'Arvor anatafsiri kuwasili kwa ujumbe huo kama ishara kali ya kisiasa: "Hili ni zoezi la kwanza... tutaonyesha Marekani kuwa Nato iko."
Harakati za wanajeshi hao zinakuja baada ya mawaziri wa mambo ya nje wa Denmark na Greenland kuzuru Washington kukutana na Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance siku ya Jumatano.
Kufuatia mkutano huo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Denmark, Lars Lokke Rasmussen alisema wakati mazungumzo hayo yakiwa ya kujenga, kumesalia "kutokubaliana kwa msingi" kati ya pande hizo mbili na baadaye kukosoa azma ya Trump ya kutaka kuinunua Greenland.
Pia unaweza kusoma:



















