Trump aiambia Cuba 'ifanye makubaliano, kabla haijachelewa'

Chanzo cha picha, Getty Images
Donald Trump ameitaka Cuba "kufanya makubaliano" au ikabiliane na matokeo, akionya kwamba mtiririko wa mafuta na pesa za Venezuela sasa utasitishwa.
Rais wa Marekani amekuwa akielekeza mawazo yake kwa Cuba tangu majeshi ya Marekani yalipomkamata kiongozi wa Venezuela Nicolás Maduro katika shambulio la Januari 3 katika mji mkuu wake.
Venezuela, mshirika wa muda mrefu wa Cuba, inaaminika kutuma takriban mapipa 35,000 ya mafuta kwa siku katika kisiwa hicho, lakini Trump amesema hilo litaisha.
"Cuba iliishi, kwa miaka mingi, kwa kiasi kikubwa cha MAFUTA na FEDHA kutoka Venezuela.
Kwa upande wake, Cuba ilitoa 'Huduma za Usalama' kwa madikteta wawili wa mwisho wa Venezuela, LAKINI HILO HALITAFANYIKA TENA!" alichapisha kwenye Truth Social on Sunday.
"HAKUTAKUWA NA MAFUTA WALA PESA KWENDA CUBA - SIFURI! Ninashauri sana wafanye mkubaliano, KABLA HAIJACHELEWA." Trump hakutaja masharti ya makubaliano au matokeo ambayo Cuba inaweza kukabiliana nayo.









