Kanye West aamriwa kulipa dola 140,000 kwa kukosa kumlipa fundi
Baraza la majaji limemuamuru rapa maarufu wa Marekani Kanye West kulipa $140,000 (£104,415) baada ya kukosa kumlipa fundi mmoja aliyemfanyia ukarabati katika jumba lake la kifahari la Malibu.
Uamuzi katika kesi hiyo huko Los Angeles ulikuja baada ya Tony Saxon kudai kwamba rapa huyo, anayejulikana pia kama Ye, hakumlipa ipasavyo kwa kazi aliyoifanya katika eneo la ufukweni na kumfukuza.
Timu ya rapa huyo ilibishana mahakamani kwamba Saxon alikuwa mkandarasi asiye na leseni ambaye "aliharibu" "kito cha usanifu" alipokuwa akifanya kazi aliyokuwa amepewa.
Saxon alikuwa ameomba fidia ya dola milioni 1.7 (£1.267 milioni) lakini jopo siku ya Jumatano lilimpa dola 140,000, pamoja na wakili na ada za mahakama.
Soma zaidi: