Mashambulizi zaidi ya Iran yaripotiwa nchini Iraq, Bahrain, na Oman
Mali mbili za mafuta zilichomwa moto karibu na bandari ya kusini mwa Iraq ya Basra, na kulazimisha shughuli kusimama katika vituo vya mafuta vya nchi hiyo. Wafanyakazi wengi waliokolewa lakini mmoja alifariki.
Nchini Bahrain, kuna moto mkubwa baada ya Iran kulenga mafuta na meli za mafuta karibu na uwanja wa ndege wa kimataifa. Moshi ni mzito kiasi kwamba mamlaka inawasihi watu kufunga madirisha yao.
Nchini Oman, kikosi cha zimamoto bado kinafanya kazi ya kudhibiti moto kwenye maeneo ya kuhifadhia mafuta kutokana na shambulizi la jana kwenye bandari ya Salalah na vile vile, Oman sasa imeagiza uhamishaji wa meli katika kituo chake cha usafirishaji mafuta kama hatua ya tahadhari.
Ni wazi kwamba Iran inakusudia kuleta msukosuko wa kiuchumi wa muda mrefu.
Kikosi chake cha Revolutionary Guard Corps pia kimeonya kwamba taasisi za fedha za magharibi sasa ni shabaha halali, baada ya shambulio dhidi ya benki ya Iran.
Benki za kimataifa zimekuwa zikifunga ofisi zao za Ghuba - HSBC ya Qatar, Citi na Standard Chartered huko Dubai - zikiwataka wafanyakazi wakae nyumbani.
Soma zaidi: