Shirika la Afya Duniani WHO laitaka Marekani kufikiria uamuzi wake
Shirika la Afya duniani limejutia hatua ya Marekani kutaka kujiondoa katika shirika hilo.
Hatua hiyo inajiri baada ya Rais Donald Trump kutia saini agizo la kutaka kujiondoa katika WHO .
Agizo hilo lilisema Marekani inajiondoa "kwa sababu ya WHO kutoshughulikia janga la Covid-19 ambalo liliibuka Wuhan, China, na majanga mengine ya afya ya ulimwengu, kushindwa kwake kupitisha mageuzi yanayohitajika haraka, na kutokuwa na uwezo wa kuonyesha uhuru kutoka kwa yasiyofaa.
Hatahivyo katika taarifa yake kwa vyombo vya habari WHO imetoa wito kwa Marekani kufikiria tena uamuzi huo.
Shirika hilo limesema kuwa ushirikiano wa Marekani umeliwezesha kuokoa idadi kubwa ya maisha mbali na kuwaokoa Wamarekani na watu wote duniani kutokana na athari za Kiafya.
Shirika hilo limeongezea kwamba Marekani ni miongoni mwa waanzilishi wa shirika hilo na imeshiriki katika usimamizi wa shirika hilo pamoja na wanachama wengine 193.
WHO limeongzea kwamba kupitia mchango wa Marekani na wanachama wengine katika kipindi cha miaka saba iliopita shirika hilo limefanikiwa kuidhinisha idadi kubwa ya mabadiliko katika historia yake ikiwa ni pamoja na kupitia ushiriki wake kikamilifu katika Bunge la Afya Duniani na Bodi ya Utendaji.
Trump alikosoa jinsi shirika hilo la kimataifa lilivyoshughulikia janga la Covid-19 na kuanza mchakato wa kujiondoa kutoka kwa taasisi hiyo ya Geneva wakati wa janga hilo.
Rais Joe Biden baadaye alibatilisha uamuzi huo.
Agizo hilo lilisema Merekani inajiondoa "kwa sababu ya WHO kutoshughulikia janga la Covid-19 ambalo liliibuka Wuhan, China, na majanga mengine ya afya ya ulimwengu, kushindwa kwake kupitisha mageuzi yanayohitajika haraka, na kutokuwa na uwezo wa kuonyesha uhuru kutoka kwa yasiyofaa. ushawishi wa kisiasa wa nchi wanachama wa WHO".
Amri hiyo ya utendaji pia ilisema hatua hiyo ilitokana na "malipo yasiyofaa" ambayo Marekani ilitoa kwa WHO, ambayo ni sehemu ya Umoja wa Mataifa.
Trump alipokuwa bado ofisini kwa mara ya kwanza alikosoa shirika hilo kwa "kuipendelea China" katika kukabiliana na janga la Covid-19.