Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kombe la Dunia 2022: Cameroon, Ghana, Morocco, Senegal na Tunisia kuiwakilisha Afrika Qatar
Timu za Cameroon, Ghana, Morocco, Senegal na Tunisia zimefuzu kutoka ukanda wa Afrika kucheza fainali za kombe la dunia ziakazopigwa baadae mwaka huu huko Qatar, kufuatia matokeo yao ya michezo ya jana.
Cameroon ikishinda ugenini 2-1 dhidi ya Algeria kwa bao la jioni na kufuzu kwa bao la ugenini baada ya mchezo wa kwanza Algeria kushinda ugenini bao 1-0. Ghana ikaiondosha Nigeria kufuatia sare ya 1-1 ugenini, mchezo wa kwanza uliopigwa Ghana, timu hizo zilienda sare ya 0-0.
Morocco ikachafua sherehe ya kumkaribisha mwanachama mpya wa Jumuia ya Afrika Mashariki, DRC baada ya kuitandika 4-1 huko Casablanca na kuiondosha kwa jumla ya mabao 5-2 kufuatia mchezo wa kwanza mjini Kinshasa kwenda sare a 1-1.
Sadio Mane akafunga penati ya ushindi Senegal ikiondosha kwa matuta Misri baada ya kulingana kwa mabao, kila mmoja akishinda kwake kwa bao 1-0.
Baada ya sare ya nyumbani ya bila kufungana, Tunisia imesongwa mbele kwa bao la ugenini ililolipata kwenye mchezo wa awali.
Bala la Ulaya
Barani Ulaya, Poland na Ureno zimefanikiwa kufuzu baada ya kushinda michezo yao ya jana usiku. Shujaa wa Ureno alikuwa Bruno Fernandes, kiungo wa Ma aliyefunga mabao mawili, Ureno ikizaba Macedonia Kaskazini mabao 2-0.
Poland ikafuzu kwenda Qatar kwa magoli ya Robert Lewandowski na Piotr Zielinski kuwapa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Sweden.
Nchi zingine zilizofuzu kutoka bara la Ulaya mpaka sasa ni pamoja na Ubelgiji, Ufaransa, England, Serbia, Uholanzi, Hispania, Croatia, Switzerland
Amerika Kusini, kati na Kaskazini
Canada ilikuwa nchi ya kwanza kufuzu kucheza kombe la dunia kutoka ukanda huu. Brazil, Argentina, Ecuador, Uruguay zimefuzu kutoka ukanda huu. Brazil ikikamilisha ratiba alfajiri ya leo kwa kuzaba 4-0 Bolivia, Argentina ikaenda sare ya 1-1 na Ecuador, Chile ikalala 2-0 dhidi ya Uruguay.
Asia
Qatar yenyewe imefuzu moja kwa moja kutokana na kuwa mwenyeji wa mashindano hayo ikiungana na Korea Kusini na Iran, Japan Saudi Arabia. Iran jana imeichapa Lebanon 2-0, Syria na Iraq zikaenda sare ya 1-1 huku UAE ikiilaza Korea Kusini kwa bao 1-0.
Mambo muhimu kufahamu kuhusu Kombe la dunia mwaka huu
Droo ya ratiba ya mashindano hayo makubwa kabisa ya soka duniani itafanyika April 1 2022, ikiwa ni miezi saba kabla ya kuanza kwa mashindano hayo Novemba 21, 2022. Mpaka kufikia April 1, ni timu 29 kati ya 32 zitakuwa zimejulikana nafasi tatu kati ya hizo 32 zitapatikana mwezi Juni. Mechi zingne zitaendelea ikiwemo ya baadae usiku leo Visiwa vya Solomon vitakuwa mwenyeji wa New Zeeland.
Fainali ya mashindano hayo yatakayo shirikisha mataifa 32 inatarajiwa kupigwa Disemba 18, 2022. Hata atakuwa mashindano ya kwanza kufanyika msahriki ya kati na yakiwa ya mwisho yakayotumia mfumo wa sasa wa kushirikisha timu 32, kabla ya kuanza kwa mfumo mpya utakaoshirikisha timu 48 kuanzia fainali za mwaka 2026.
Orodha kamili ya timu zilizofuzu mpaka sasa
1: Argentina
2: Ubelgiji
3: Denmark
4: Cameroon
5: Brazil
6: England
7: Croatia
8: Ujerumani
9: Canada
10: Ecuador
11: Ufaransa
12: Japan
13: Iran
14: Morocco
15: Ghana
16: Uruguay
17: Serbia
18: Korea Kusini
19: Saudi Arabia
20: Poland
21: Ureno
22: Qatar
23: Uholanzi
24: Tunisia
25: Hispania
26: Switzerland
27: Senegal