Brittney Griner: Je mchezaji wa mpira wa vikapu wa Marekani anawezaje kutoweka tu hivyo?

Chanzo cha picha, Getty Images
Bila shaka yeye ndiye mchezaji bora wa kike wa mpira wa vikapu wa wakati wote, na amezuiliwa huko Moscow wakati wa vita.
Mashabiki wanataka kujua ni kwa nini watu wengi zaidi hawajali kuhusu hilo.
Katika mojawapo ya matukio ya mwisho kuonekana hadharani ya Brittney Griner, yaliyonaswa kwenye CCTV, mchezaji huyo wa Marekani wa mpira wa vikapu anaonekana akipitia vituo vya ukaguzi usalama wa uwanja wa ndege akifuata mkoba mdogo, mweusi.
Bi Griner, nyota wa Phoenix Mercury, alikuwa ametua kwenye uwanja wa ndege wa Sheremetyevo, nje ya Moscow, kucheza msimu mwingine na ligi ya Urusi.
Katika picha za usalama, amevaa viatu vya riadha, suruali nyeusi ya jasho na kofia nyeusi iliyoandikwa "Black Lives for Peace" mgongoni, nywele zake nyeusi zikininginia chini ya mabega yake.
Unaweza pia kusoma
- YA MSINGI:Mzozo wa Ukraine: Kwanini Urusi inaivamia Ukraine na Putin anataka nini?
- UFAFANUZI:Mzozo wa Ukraine: Swift ni nini na kwa nini kuipiga marufuku Urusi ni muhimu sana?
- UCHAMBUZI:Mzozo wa Ukraine: Putin humsikiliza nani?
- KWENYE RAMANI:Uvamizi wa Ukraine: Shambulio la Urusi kwenye ramani
- ZELENSKY:Volodymyr Zelensky: Mfahamu rais wa Ukraine aliyeacha umaarufu wake wa TV na kuingia kwenye siasa
- PUTIN:Vladimir Putin: Rais wa Urusi aliyeagiza shambulio Ukraine
- SILAHA:Mzozo wa Ukraine:Makombora ya stinger na silaha nyingine kali zinazotumiwa Ukraine
Akiwa na futi 6 na inchi 9 - mrefu hata kulingana na viwango vya mpira wa vikapu - anakuwa juu ya mawakala wa forodha na wasafiri wengine.
Katika video nyingine, anaonekana ameketi mbele ya mwanamume, anayeonekana kuwa wakala wa forodha, akitikisa kichwa "hapana".
Kisha, hakuna kitu kinachoendelea - mpaka polisi mpiga picha wa Kirusi alipojitokeza kwenye televisheni ya serikali wiki iliyopita.
Bi Griner, 31, anaaminika kukamatwa na mamlaka ya Urusi kwa tuhuma za dawa za kulevya.
Mwezi mmoja baada ya kuzuiliwa kwake, hakuna kinachojulikana kuhusu hali yake.
Kutokuwa na uhakika kuhusu hatima yake kumechochea uungwaji mkono mwingi kwa mchezaji huyo, ambaye anachukuliwa na mashabiki na wachambuzi wa michezo vile vile kuwa labda mchezaji bora zaidi wa kike wa mpira wa vikapu wakati wote.
Na pia imezua hisia za hasira miongoni mwa baadhi ya mashabiki wanaosema jibu la kuzuiliwa kwa Bi Griner limenyamazishwa kwa kushangaza.
Mashabiki na wataalamu wanasema kwamba umakini ambao amepewa ikilinganishwa na wachezaji wa kiume hufichua ukosefu wa usawa wa kijinsia wa muda mrefu katika michezo ya kitaaluma.
"Kama huyu angekuwa mchezaji wa NBA [ligi ya kitaaluma ya wanaume] wa kiwango chake... hii ingekuwa kwenye jalada la sio tu kila ukurasa wa michezo bali kila ukurasa wa vyombo vya habari duniani," alisema Tamryn Spruill, mwandishi wa habari za michezo ambaye anaandika. kitabu juu ya WNBA na Bi Griner.

Chanzo cha picha, Getty Images
Brittney Griner, mkongwe wa miaka tisa katika ligi - ndiye "bora zaidi", alisema Melissa Isaacson, mwandishi wa michezo na profesa katika Chuo Kikuu cha Northwestern katika jimbo la Illinois la Marekani.
"Yeye ni kila kitu mfano wa Tom Brady wa mchezo wake," Bi Isaacson alisema.
"Unaweza kubishana kwa usahihi kwamba yeye ni mmoja wa wachezaji bora zaidi ulimwenguni."
Mzaliwa wa Houston, Texas, alipata udhamini wa mpira wa vikapu hadi Chuo Kikuu cha Baylor ambapo aliiongoza timu hiyo kwenye ubingwa wa kitaifa.
Sasa ni mmoja wa wachezaji mashuhuri zaidi wa WNBA katika historia, anayezingatiwa sana kuwa mchezaji bora mshambuliaji kwenye ligi.
Wachache wametimiza kile Bi Griner amefanya - kushinda ubingwa wa chuo kikuu, mataji ya WNBA na Euroleague na medali ya dhahabu ya Olimpiki.
Na, ni maarufu sana kwa uwezo wake wa kupiga mbizi ambao ni wa kipekee.
Nje ya uwanja, pia ameonekana kama aliyechukua njia mpya, akionekana kama anayeshiriki mapenzi ya jinsia moja akiwa na umri wa miaka 22, muda mfupi tu kabla ya kuanza kushiriki mchezo wa kulipwa.
Kisha akawa mteule wa kwanza wa jumla katika WNBA mwaka huo na, punde baadaye, mchezaji wa kwanza ambaye anashiriki mapenzi ya jinsia moja waziwazi na kuidhinishwa na Nike.
"Kabla ya Griner, kulikuwa na kama giza kwenye ligi, ambapo ilikuwa ni kama "usiseme chochote juu ya wapenzi wa jinsia moja" Bi Spruill alisema.
Na yeye alikuwa ni kama yuko tayari kumaliza ukimya huo, "huyu ndiye mimi"
"BG daima imekuwa mmoja wa waanzilishi," mchezaji mwenza wa Griner, Diana Taurasi alisema.

Chanzo cha picha, Getty Images
Licha ya hayo yote, Bi Griner alipata kazi ya pili, na hiyo ndiyo sababu alisafiri kwa ndege hadi Urusi - kuchezea timu ya EuroLeague UMMC Ekaterinburg, ambako amekuwa akifanyakazi tangu 2014 wakati msimu ulikuwa chini Marekani.
Takriban nusu ya wachezaji wa WNBA hucheza nje ya nchi nyakazi ambazo msimu uko chini.
Kwa walio wengi, ni njia ya kuongeza mapato yao ya ndani: Wachezaji wa WNBA hupokea takriban mara tano zaidi nchini Urusi kuliko wanavyopokea Marekani.
"Kama angekuwa Steph Curry au LeBron James, hangekuwa hapo hata kidogo kwa sababu angekuwa akipata pesa za kutosha," Bi Spruill alisema.
Wenzake Bi Griner katika ligi ya wanaume wanapata zaidi ya mara 200 ya mshahara wa juu zaidi wa WNBA.
Kufuatia uvamizi wa Urusi dhidi ya Ukraine tarehe 24 Februari, EuroLeague ilizisimamisha timu zote za Urusi na maafisa wa Marekani na WNBA walianza kuwaita wachezaji walio nje ya nchi.
Lakini ilikuwa ni kuchelewa sana kwa Brittney Griner, ambaye inaaminika aliingia Urusi wiki moja mapema, tarehe 17 Februari, ingawa muda bado haujafahamika.
Huduma ya Forodha ya Shirikisho la Urusi ilisema katika taarifa kwa vyombo vya habari kwamba mbwa wa kunusa aliongoza mamlaka kupekua mizigo ya mchezaji wa mpira wa vikapu wa Marekani na kwamba imepata cartridges ya vape yenye mafuta ya bangi.
Shirika la habari la serikali la Urusi, Tass, lilimtaja mchezaji huyo kuwa ni Bi Griner.
Mamlaka ya Urusi ilithibitisha tu kuzuiliwa kwake wiki ya tatu ya Machi, ingawa walifichua kwamba alisimamishwa kwenye uwanja wa ndege mnamo Februari.
Ambapo anazuiliwa, na chini ya hali gani, haijulikani hadharani.

Chanzo cha picha, Getty Images
Mamlaka ya Marekani na wawakilishi wa Brittney Griner wamekuwa kimya zaidi isipokuwa kusema wanafanya kila namna kumrudisha nyumbani.
Msemaji wa idara ya serikali alithibitisha kuzuiliwa kwa mchezaji huyo, akiambia BBC kuwa "wanafahamu na wanaifuatilia kwa karibu na kesi hii".
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken alisema wiki iliyopita kwamba maafisa wa Marekani "wanafanya kila wawezalo" kumsaidia.
"Kuna mengi tu nisiyoweza kusema kutokana na masuala ya faragha wakati huu," Bw Blinken alisema.

Chanzo cha picha, Getty Images
Wakala wa Bi Griner, Lindsay Colas, amesema alikuwa na "mawasiliano ya karibu" na mchezaji huyo na wakili wake nchini Urusi, lakini hakuweza kuzungumza zaidi.
Ingawa hakuna dalili kwamba kukamatwa kwa Bi Griner kulihusishwa na uvamizi wa Ukraine, baadhi ya maafisa wa Marekani wameonyesha kuwa uhusiano mbaya kati ya Marekani na Urusi unaweza kuhatarisha kurejea kwake akiwa salama.
"Hatutaki Bi Griner kuwa kibaraka katika vita vya kisiasa vinavyopiganwa kote ulimwenguni hivi sasa," alisema mbunge wa Marekani John Garamendi, mjumbe wa kamati ya huduma za silaha kutoka Bunge la Wawakilishi.
"Vita vya Ukraine kimsingi vimekatiza uhusiano wa kidiplomasia kati ya Marekani na Urusi," Bw Garamendi alisema.
"Hilo litazidisha suala hili.
Urusi hadi sasa imezuia ufikiaji wa ubalozi kwa Brittney Griner kwa ubalozi wa Marekani, alisema.
Anaweza kufungwa jela hadi miaka 10 iwapo atapatikana na hatia kwa makosa ya dawa za kulevya.
Aidha, ubalozi wa Marekani nchini Urusi haukujibu ombi la maoni.















