App za Facebook, Instagram, WhatsApp zashindwa kupakia na kupakua picha

Chanzo cha picha, Getty Images
Baadhi ya watumiaji wa Facebook, Instagram na WhatsApp walishindwa kuweka picha, video na mafaili.
Facebook, inayomiliki App zote tatu, imesema inafahamu kuhusu tatizo hilo na ilikuwa ''ikifanyia kazi ili kurudisha kila kitu sawa haraka iwezekanavyo''.
Mitandao ya kijamii, ina mabilioni ya watumiaji wake ulimwenguni.
Washindani wake Twitter pia walikuwa na tatizo kwa watumiaji wake kushindwa kutuma ujumbe wa moja kwa moja au kupokea taarifa kuhusu ujumbe ulioingia.
Kampuni iliomba radhi kwa dosari hiyo kupitia ukurasa wake wa Twitter wakisema kuwa wanashughulikia tatizo hilo.
Watumiaji bado waliweza kuweka ujumbe kwenye twitter na ujumbe wa hashtag #instagramdown ukaanza kushika kasi mtandaoni wengi wakitumia kueleza matatizo ya mshindani wake.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe
App ya Facebook Messenger, ambayo huwa inapakuliwa kivyake, nayo ailiathirika.
Mwezi Machi, Facebook na Instagram ilipata changamoto za kiteknolojia ambayo ilidumu wa muda. Matatizo pia yalikumba app zote mbili sambamba na Whats App mwezi Aprili.
Facebook ina watumiaji zaidi ya bilioni 2.3 kwa mwezi wanaotumia app hiyo na Instagram ina watumiaji bilioni moja.













