Msumbiji: Athari za Kimbunga Kenneth kwa Picha

Chanzo cha picha, AFP
Kimbunga kikali kimeharibu maelfu ya nyumba na kuwaua makumi ya raia nchini Msumbiji.
Kimbunga Kenneth kiliwasili siku ya Alhamisi kikiwa upepo wenye kasi wa kilomita 220 kwa saa
Imetabiriwa kwamba hali ya hewa nchini humo itasababisha mvua kubwa zaidi ya ile iliojiri baada ya kimbunga Idai Idai, ambacho kilisababisha zaidi ya watu 900 kupoteza maisha yao katika mataifa ya Msumbiji , Malawi na Zimbabwe mwezi uliopita.

Chanzo cha picha, OCHA/Saviano Abreu/via REUTERS
Pemba, mji mkuu wa jimbo la Cabo Delgado limepata mvua yenye kiwango cha zaidi ya milimita 2 na kusababisha barabara kuwa mito.

Chanzo cha picha, Reuters


Chanzo cha picha, Reuters


Chanzo cha picha, Reuters
hatari hiyo ya mafuriko ilisababishwa na kimbunga Kenneth kilichopiga eneo hilo mwisho wa msimu wa mvua wakati ambapo mito ilikuwa imejaa maji , kulingana na afisi ya Umoja wa mataifa inyosimamia maswala ya kibinaadamu (Ocha) .

Chanzo cha picha, AFP
Mafuriko yamesababisha uharibifu wa miundo msingi na kuzuia usambazaji wa misaada .

Chanzo cha picha, STRINGER/AFP
Kimbunga Kenneth tayari kimefanya uharibifu katika taifa la kisiwani la Comoros

Chanzo cha picha, AFP
Msemaji wa Ocha Saviano Abreu alisema kuwa hali katika miji ya Macomia na Quissanga ilikuwa mbaya, akiongezea kuwa kulikuwa na wasiwasi katika kisiwa cha Ibo kilichozungukwa na maji.

Chanzo cha picha, NASA
.












