Ofwono Opondo: Uganda ni salama kushinda Marekani

Jean-Paul Mirenge (kushoto) na Kimberly Endicott

Chanzo cha picha, Wild Frontiers Uganda

Muda wa kusoma: Dakika 2

Msemaji wa serikali ya Uganda amesema kuwa rais wa Marekani anafaa kutatua matatizo ya taifa lake badala ya kuingilia maswala ya Uganda.

Ofwono Opondo alikuwa akijibu chapisho la mtandao wa Twitter kutoka kwa rais Donald Trump ambalo linasema kuwa watu hawatatamani kwenda Uganda hadi pale watekaji nyara wa raia wa Marekani pamoja na mwongozaji wake watakapokamatwa.

Wawili hao waliachiliwa siku ya Jumapili.

Bwana Opondo alijibu kupitia mtandao wa Twitter akisema kuwa kuna vifo vingi vya bunduki nchini Marekani zaidi ya utekaji nyara nchini Uganda.

Ruka X ujumbe, 1
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 1

Ruka X ujumbe, 2
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 2

Aliongezea kuwa Uganda itaendelea kuimarisha usalama wake.

Kufuatia utekaji nyara wa wawili hao rais Trump alisema kuwa utekaji nyara huo huenda ukaathiri utalii nchini Uganda akiongezea kuwa watekaji hao ni sharti wakamatwe kabla ya watalii kuzuru taifa hilo.

Wawili hao walikamatwa wakizuru mbuga ya wanyama pori ya Queen Elizabeth National Park

Chanzo cha picha, Getty Images

Awali rais Musevei alikuwa ametuma ujumbe wa Twitter akisema kuwa taifa lake liko salama kwa raia wa Uganda na watalii.

Aliwalaumu wahalifu wachache kwa visa kama hivyo .

Je kikombozi kilitolewa?

Wawili hao walitekwa wakati walipokua wakitembea katika mbuga ya Malkia Elizabeth jioni ya tarehe 2 Aprili.

Maafisa wa polisi nchini Uganda walisema kuwa watekaji hao walitumia simu moja kuitisha $500,000 (£383,435) kama kikombozi.

Hatahivyo haijulikani iwapo walilipwa.

Ruka X ujumbe, 3
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 3

Operesheni ya kuwatafuta

Operesheni ya pamoja ya usakaji iliofanywa na wanajeshi, mamlaka ya wanya pori Uganda na kitengo cha polisi wa Utalii ilianzishwa ili kumuokoa bi Endicott na bwana Mirenge.

Ramani ya mbuga ya wanyama pori ya Queen Elizabeth National Park

Lakini msemaji wa serikali alituma ujumbe wa Twitter kwamba waliokolewa na vikosi vya serikali ya Uganda nchini DRC na kwamba walikuwa salama salmin katika mpaka wa DRC na Uganda.

Chombo cha habari cha France-Presse hatahivyo kiliinukuu kampuni ya Frontiers Safaris- ikisema kuwa wawili hao waliachiliwa baada ya kikombozi kulipwa watekaji hao.

Ruka X ujumbe, 4
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 4

Baada ya utekaji huo maafisa wa polisi walikuwa wamesema kuwa kundi moja la watu wanne waliokuwa wamejihami kwa bunduki waliwakamata watalii hao na kuwateka wawili wao kabla ya kutoweka nao.

Watalii wengine waliodaiwa kuwa wanandoa wawili waliokolewa baadaye.