Wakenya wahoji taarifa iwapo ni mara ya kwanza chui adimu mweusi ameonekana kwa zaidi ya miaka 100

Chanzo cha picha, BURRARD-LUCAS PHOTOGRAPHY
Chui adimu mweusi ameonekana katika eneo la kati nchini Kenya.
Jina 'Black Panther' kama wanavyofahamika chui wengine wa aina hiyo, wamepata umaarufu kutokana na filamu Marekani ambayo inatazamwa pakubwa kote - lakini kupata fursa ya kumuona kwa uhalisi ni kitu adimu sana.
Mpiga picha wa wanyama pori, Will Burrard-Lucas amefanikiwa kumuona - na inadhaniwa kwamba ni mara ya kwanza kwa mtu yoyote kumpiga picha chui wa rangi kama hiyo barani Afrika katika muda wa miaka 100.
Kuna picha chache za kiumbe huyu, ambaye ni wa siri.
Will alipata fununu kuhusu chui huyo mweusi 'Black panther' - neno linalotumika kumaanisga chui mweusi ikitegemea anatokea sehemu gani duniani, - kuwa ameonekana katika kambi ya wanyama pori huko Laikipia.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 1
Baada ya kufuata alama za miguu ya chui huyo katika njia aliyotumia, na kwa usaidizi wa muongozaji wa eneo hilo, Will alijikita sehemu moja alikutundika kamera zake.
"Nimezoea kuweka mitego ya kamera, na huwa mara nyingine sipati chochote, kwasababu ni kama bahati nasibu tu, hujui iwapo mnyama unayetaka kumpiga picha atakuja katika njia ulioweka mtego wako wa kamera."
Walikuwa hawana hakika iwapo njia waliofuata ndio njia iliyofuatwa na chui huyo mweusi au ni chui wa kawaida tu.
"Huwa sina tamaa sana, na baada ya usiku kadhaa, sikumpata chui huyo na nilianza kufikiria, nitakuwa nimepata bahati hata angalau nikapata picha ya chui wa kawaida tu."

Chanzo cha picha, Image copyrightBURRARD-LUCAS PHOTOGRAPHY
Lakini kwa siku wa nne, alibahatika.
Na katika picha zote, chui huyo mweusi alionekana peke yake.
Watafiti wanadokeza kuwa melanin au rangi ya ngozi, ni kinyume cha ulemavu wa ngozi yaani albinism, na mara nyingi hutokea kutokana na jeni inayosababisha kuongezeka kwa kiwango cha rangi mwilini au za manyoya ya mnyama ili kumfanya awe mweusi.
Lakini je hii ni mara ya kwanza kwa mnyama huyo kuonekana au kunakiliwa kuonekana katika miaka 100 kama inavyodaiwa? Wakenya wamelihoji hilo kupitia mitandao ya kijamii:
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 2
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 3













