New York Times lashutumiwa kwa kuchapisha picha za maiti katika shambulio Kenya

Shambulio Nairobi

Chanzo cha picha, EPA

Muda wa kusoma: Dakika 1

Gazeti la New York Times limeshutumiwa vikali kwa kuchapisha picha za miili ya watu waliopoteza maisha katika shambulio la hoteli ya kifahari ya DusitD2 jijini Nairobi.

Wahalifu wenye silaha za moto na mabomu walivamia viunga vya hoteli hiyo Jumanne saa 9 alasiri.

Gazeti hilo lenye makao makuu yake nchini Marekani limechapisha picha za marehemu wakionekana dhahiri kuwa na matundu ya risasi kwenye miili yao na kulowa damu.

Wakenya walimimina hasira na kukirihishwa kwao kwa hatua hiyo ya NYTimes kwa kuandika ujumbe katika mitandao ya kijamii ikwemo Twitter.

Baadhi hata walilinganisha namna walivyoripoti matukio ya uhalifu nchini Marekani tofuati na walivyofanya kwa mkasa huu Kenya.

Ruka X ujumbe, 1
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 1

Ruka X ujumbe, 2
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 2

Wameeleza kwamba hatua ya gazeti hilo ilikosa heshima.

Ruka X ujumbe, 3
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 3

Baada ya shutuma hizo kushika kasi, uongozi wa gazeti hilo ulitoa taarifa ya kujitetea wakisema lengo lao ni "kuonesha uhalisia wa tukio zima japo picha zinaweza kuwa za kuogofya."

Wameendelea kufafanua kwamba wao hufanya vivyo hivyo wanaporipoti matukio kama hayo kwengineko duniani.