Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Unafahamu nini kuhusu vito vya Afrika vilivyoporwa na wakoloni?
Wakati wa ukoloni Afrika, maelfu ya vitu vya thamani na vya maana kubwa kitamaduni vilitwaliwa na mataifa ya magharibi na sasa vinapatikana katika makumbusho Ulaya na Marekani.
Lakini sasa, Ufaransa imezindua ripoti ambayo inatoa wito kwa turathi hizo za Afrika zilizo kwenye makumbusho nchini humo kurejeshwa Afrika. Hii imejiri huku wasimamizi wa makumbusho mengine makuu Ulaya wakisema wako tayari kuirejeshea Nigeria baadhi ya vitu vya thamani vilivyo Ulaya, lakini kwa mkopo.