Watu waliojihami wamteka mfanyakazi wa shirika la misaada pwani ya Kenya

RAMANI
Muda wa kusoma: Dakika 1

Kundi la watu wasiojulikana waliojihami wamemteka mwanamke mfanyakazi wa shirika la misaada, raia wa Italia kutoka kusini mashariki mwa Kenya, Polisi inasema.

Wanaume hao wanaoarifiwa kujihami kwa bunduki, "wamefyetua risasi kiholela" kabla ya kumteka msaidizi huyo mwenye umri wa miaka 23 nje ya mji wa pwani Malindi.

Watu watano pia wanaarifiwa kujeruhiwa na wamepelekwa hospitalini, mmoja kati yao akiwa yuko katika hali mahututi.

Haijajulikana wazi ni kwanini shambulio hilo limetokea na waliolitekeleza ni akina nani, polisi wanasema.

Hatahivyo, polisi imeeleza kwamba wanalichukulia tukio hilo, lililotokea mwendo wa saa mbili Jumanne usiku kama la kigaidi.

Katika ujumbe kwenye Twitter, idara ya Polisi nchini imesema wanaume hao walikuwa wamebebea bunduki aina ya AK47 walizozitumia kulivamia jumba la kibiashara la Chakama katika kaunti ya Kilifi pwani ya Kenya nje kidogo ya mji wa Malindi.

Polisi kwa sasa wametawanywa kuwasaka wahalifu hao.

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe