Lori laning'inia kwa njia ya ajabu kwenye daraja juu ya barabara Australia

A truck hangs off an overpass bridge with its contents spilled across the motorway below

Chanzo cha picha, VicRoads/Twitter

Muda wa kusoma: Dakika 1

Lori hili lilikuwa linasafirisha bidhaa zilizotokana na mayai na nyama nyama ya kuku nchini Asutralia pale haya yalipotokea.

Loli hilo lilibaki kuning'inia kwenye daraja juu ya barabara moja katika jimvo la Victoria.

Ajali hiyo ilisababisha barabara kufungwa na madereva wengi kukwama kwenye foleni katika barabara ya Calder Freeway kaskazini mwa mji wa Melbourne.

Bidhaa zilizokuwa zinasafirishwa na lori hilo zilimwagika na kutapakaa kwenye barabara iliyoko chini.

Vyombo vya habari nchini humo vinasema dereva wa lori hilo amekimbizwa hospitalini, lakini haonekani kuwa na majeraha yanayotishia maisha yake.

Maafisa wanafanya uchunguzi kubaini chanzo cha ajali hiyo, lakini wanasema kuna uwezekano lori hilo liligonga kizuizi pembeni mwa barabara na kupinduka.

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe