Marekani yapendekeza sheria ya kupiga marufuku wahamiaji haramu

Majeshi ya Marekani katika mpaka wa taifa hilo na Mexico

Chanzo cha picha, AFP/Getty

Maelezo ya picha, Majeshi ya Marekani katika mpaka wa taifa hilo na Mexico
Muda wa kusoma: Dakika 2

Wahamiaji wanaoingia nchini Marekani kupitia mpaka wa kusini hawatapewa hifadhi tena chini ya sheria mpya ya uhamiaji, utawala wa Trump umesema.

Tangazo hilo lilitolewa na idara ya haki na usalama wa kitaifa linasema sheria hiyo mpya itakomesha visa vya wahamiaji waliyokiuka sheria kuingia Marekani.

Rais ana uwezo wa kupiga marufuku wahamiaji kwa ''maslahi ya taifa'' ilisema tangazo hilo.

Suala la uhamiaji lilikuwa ajenda kuu ya kampeini ya rais Trump katika uchaguzi wa mwaka 2018 wa katikati ya muhula.

Trump amekuwa akikabiliana na msafara wa maelfu ya wahamiaji kutoka Amerika ya Kati ambao wamekuwa wakitaka kuingia nchini Marekani kupitia mpaka wa kaskazini.

Aliamuru majeshi kushika doria katika mpaka huo kama hatua aliyosema ni ya kulinda nchi dhidi ya ''wavamizi''

Kaimu mwanasheria mkuu Matthew Whitaker na mkuu wa usalama wa kitaifa Kirstjeb Nielsen walitangaza kile kinachojulikana kama sheria ya mpito siku ya Alhamisi.

Katika taarifa ya pamoja viongozi hao walisema rais ana ''mamlaka ya kufutilia mbali uhamiaji wote''endapo wahamiaji watakiuka vikwazo vinavyodhibiti shughuli zao.

Pia wanasema hilo linaweza kufanyika ikiwa uwepo wao nchini utahatarisaha usalama wa Wamarekani.

Doria ya mpakani zinashikiliwa na maafisa wa Marekani

Chanzo cha picha, AFP/Getty

Maelezo ya picha, Walinzi wa Marekani wanashika doria karibu na ukuta unaogawanya mpaka kati ya Marekani na taifa jirani

Rais Trumpa anatarajiwa kuidhinisha agizo hilo kuwa sheria.

Hatua hiyo imepingwa vikali na muungano unaotetea haki ya raia ukisema ''inakiuka sheria''.

Maafisa wa muungano huo walisema "Sheria za Marekani zinawaruhusu watu kuomba hifadhi wakiwa nchini mwao ama wakiwa katika kituo cha mpakani''

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe

Presentational white space

Chini ya katiba ya Marekani wahamiaji wana haki ya kusikilizwa hasa wanaposema wanahofia usalama wao katika taifa waalotokea.

Wale wanaotafuta hifadhi huwa watoroka nchini mwao kwa kuhufia maisha yao.

Chini ya sheria ya kimataifa watu hao wanatambuliwa kama wakimbizi.

Mhamiaji anayetafuta hifadhi ambaye sasa anasadikiwa kuwa nchini Marekamu kwa njia haramu- pia anashathili kusikilizwa

Juhudi zilizopita za utawala wa Trump kukabilia suala la wahamiaji zimekosolewa vikali kisiasa na kisheria

Mwezi Juni mwaka huu rais alitia saini amri ya utendaji kuahidi "kuweka familia pamoja" katika kituo cha kuwashikilia wahamiaji, baada ya wazazi na watoto kutenganishwa

Siku kadhaa baadae mahakama ya juu zaidi ilidumisha marufuku ya usafiri iliyotolewa na utawala wa Trump dhidi ya mataifa kadhaa ya Kiislamu.

Mwanzoni mahakama kadhaa ziliamua kwa hatua hiyo ilikiuka katiba ya marekani.