Kwa Picha: Mazishi ya dada yake rais wa Tanzania John Magufuli yalivyokuwa Chato, Geita, Raila Odinga ahudhuria
Kiongozi mkuu wa upinzani nchini Kenya, Waziri Mkuu wa zamani Raila Odinga aliungana na viongozi wastaafu wa Tanzania katika mazishi ya dadake Rais wa Tanzania Joseph Magufuli, Monica Magufuli.
Mazishi hayo yalifanyika katika kijiji cha Mlimani Chato mkoani Geita.

Chanzo cha picha, IKULU, Tanzania

Chanzo cha picha, Ikulu
Bi Monica alifariki dunia asubuhi ya tarehe 19 Agosti, 2018 katika hospitali ya Bugando Jijini Mwanza alikokuwa akipokea matibabu.
Rais Magufuli alikuwa amemtembea hospitalini Magufuli Jumamosi akiwa amelazwa katika Chumba cha uangalizi Maalum ICU.

Chanzo cha picha, Ikulu

Chanzo cha picha, RAILA ODINGA/TWITTER
Rais Magufuli akiwa anazungumza jambo na Rais Mstaafu wa awamu ya pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi mara baada ya kumaliza mazishi.

Chanzo cha picha, Ikulu

Chanzo cha picha, Ikulu
Rais Magufuli akiweka shada la maua katika kaburi la dada yake baada ya mazishi.

Chanzo cha picha, Ikulu

Chanzo cha picha, Ikulu

Chanzo cha picha, Ikulu
Rais Magufuli akiwa na Mama yake mzazi Suzana Magufuli wakati wakitoa heshma za mwisho katika jeneza.

Chanzo cha picha, Ikulu
Magufuli akiweka udongo ndani ya kaburi.

Chanzo cha picha, Ikulu
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akitoa heshma za Mwisho katika jeneza.

Chanzo cha picha, Ikulu
Baba Askofu mkuu Mwandamizi Yuda Thaddeus Ruwaichi akiongoza Misa ya kumuombea Marehemu Monica Magufuli Chato mkoani Geita.
Picha zote: Ikulu, Tanzania












