Mtalii kutoka China auawa na kiboko akipiga picha katika ziwa Naivasha Kenya

Mtalii kutoka China, Chang Ming Chuang mwenye umri wa miaka 66 amefariki baada ya kuvamiwa na kiboko Jumamosi jioni.
Mamlaka ya hifadhi ya wanyama pori ya Kenya imeandika kwenye mtandao wake wa Twitter kuwa raia huyo kutoka China alivamiwa na kiboko wakati alipokuwa anampiga picha katika ziwa Naivasha eneo la sopa resort huko Nakuru.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe
Huku mwenzie Wu Peng Te mwenye umri wa miaka 62 amenusurika lakini bado yupo hospitali kwa ajili ya matibabu.
Kiboko huyo bado anatafutwa.








