Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mtalii kutoka China auawa na kiboko akipiga picha katika ziwa Naivasha Kenya
Muda wa kusoma: Dakika 1
Mtalii kutoka China, Chang Ming Chuang mwenye umri wa miaka 66 amefariki baada ya kuvamiwa na kiboko Jumamosi jioni.
Mamlaka ya hifadhi ya wanyama pori ya Kenya imeandika kwenye mtandao wake wa Twitter kuwa raia huyo kutoka China alivamiwa na kiboko wakati alipokuwa anampiga picha katika ziwa Naivasha eneo la sopa resort huko Nakuru.
Huku mwenzie Wu Peng Te mwenye umri wa miaka 62 amenusurika lakini bado yupo hospitali kwa ajili ya matibabu.
Kiboko huyo bado anatafutwa.