Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Trump atangaza atakutana na Kim Jong-un Singapore
Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kwamba atakutana na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un Singapore tarehe 12 Juni.
Bw Trump aliushangaza ulimwengu Aprili alipotangaza kwamba amekubali mwaliko wa kukutana moja kwa moja na Bw Kim.
Wawili hao awali walikuwa wamerushiana matusi na vitisho.
Ufanisi huo ulitokea baada ya mazungumzo ya kihistoria kati ya viongozi wa Korea Kaskazini na Korea Kusini.
Trump ametangaza hilo saa chache baada yake kuwakaribisha nyumbani Wamarekani watatu ambao wamekuwa wakizuiliwa na Korea Kaskazini ambao waliachiliwa huru na kuruhusiwa kurejea nyumbani.
Waliachiliwa wakati wa ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Mike Pompeo mjini Pyongyang kupanga na kufanya mazungumzo zaidi kuhusu mkutano huo wa Trump na Kim Jong-un.