Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mkufu wa Almasi wauzwa dola milioni 33.7 mjini Geneva
Mkufu wa almasi kwa karati 163 ambao ni mkubwa zaidi wa aina yake kuuzwa, sasa umeuzwa kwa dola milioni 33.7 katika mnada huko Geneva.
Mkufuku huo ulichongwa kutoka kwa almasi ya karati 404 iliyopatikana nchini Angola.
Mkufu uliokamilika ulitengenezwa kutoka kwa dhahabu nyeupe, almasi na mawe ya thamani.
Uliuzwa katika hoteli ya Four Seasons mjini Geneva baada kuwekwa kwenye maonyesho huko Hong Kong, London, Dubai na New York.
Bei ya mkufu ilikuwa ya juu kuliko ile iliyotarajiwa ya dola milioni 30.
Aliyeununua mkufu huo hajatajwa.