Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Rais Paul Biya alaani vurugu, Cameroon
Rais wa Cameroon, Paul Biya amelaani ghasia zilizotekelezwa na pande zote baada ya polisi kuwapiga risasi na kuwauwa watu nane wakati wa maandamano ya raia wa nchi hiyo wanaozuungumza kiingereza wanaotaka kujitenga kuwa na eneo lao.Watu wanane wamejeruhiwa katika ghasia hizo.
Ghasia hizo zimetokea wakati wa maadhimisho ya miaka miaka hamsini na sita tangu kujumuishwa kwa jimbo la wazungumzaji wa kiingereza ndani ya Cameroon.
Wazungumzaji wa lugha ya Kiingereza ambao ni wachache wamekuwa wakiandamana takriban mwaka sasa kwa kile wanachosema kubaguliwa katika mfumo wa elimu na sheria.