Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kobe 2500 wakamatwa kwa kumilikiwa kinyume na sheria India
Maafisa katika mji wa Tamil Nadu nchini India wamesema wamefanikiwa kukamata zaidi ya kobe 2,500 waliokuwa wanamilikiwa kinyume na sheria.
Kobe hao wamepatikana wakati wa msako mkali katika mji wa Chennai.
Mtu mmoja anashikiliwa na polisi kwa mahojiano.
Kobe hao kwa pamoja wanakadiriwa kuwa na bei ya dola 40,000.
Kuna uhitaji mkubwa wa kobe Asia ya Kaskazini, ambapo hutumika kwa shughuli mbalimbali ikiwemo chakula.