Trump aitaka Urusi kuwacha kuivuruga Ukrain

Donald Trump (left) with Andrzej Duda in Warsaw, 6 July

Chanzo cha picha, EVN

Maelezo ya picha, Trump (kushoto) na rais wa Poland Andrzej Duda

Rais wa Marekani Donald Trump ametoa wito kwa Urusi kuacha kuivuruga Ukrain na nchi zingine, na kuacha kuungia mkono tawala dhalimu kami zile za Styria na Iran.

Akiongea akiwa mji mkuu wa Poland Warsaw, Trump aliitaka Urusi kujiunga na mataifa yenye kuwajibika.

Urusi imepinga matamshi hayo ya Trump.

Mr and Mrs Trump arrive in Hamburg

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Bwana Trump akiwasili Hamburg kwa mkutano wa G20

Rais huyo wa Marekani amesafiri kuenda mjini Hamburg kuhudhuria mkutano wa G20 ambapo atakutana na rais wa Urusi kwa mara ya kwanza.

Mjini Warsaw alihutubia umati mkubwa uliokuwa ukimshangilia

Aliisifu Poland kama nchi iliyo tayari kulinda uhuru wa magharibi.

People holding portraits of US President Donald Trump and Polish President Andrzej Duda wait at Krasinski Square in Warsaw, 6 July

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Watu wanaosikiliza hotuba ya trump Poland

Bwana Trump aliitaka Urusi kuungana na nchi zinaowajibika katika vita dhidi ya adui mmoja.

Msemaji wa serikali ya Urusi Dmitry Peskov alisema kuwa Urusi haijakubali kuwa inavuruga eneo hilo.

Anti-capitalism activists wearing masks of UK Prime Minister Theresa May (L) and US President Donald Trump protest in Hamburg, 6 July

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Waziri mkuu wa Uingereza Theresa May na rais wa Marekani Donald Trump wakikejeliwa Hamburg on Thursday

Trump ametofautiana na baadhi ya nchi za ulaya kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa na biashara,

Mashirika ya kutoa misaada yatarajiwa kufanya maandamano mjini Hamburg kuwakata viongozi kujitahidi zaidi kumaliza kutokuwepo usawa.

Activists arrive at Hamburg central railway station, 6 July

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Waandamani wawasili kwa traini mjini Hamburg
Polish First Lady Agata Kornauser-Duda (R) and US First Lady Melania Trump (L) during a tete-a-tete meeting in Belweder Palace in Warsaw, 6 July

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Melania Trump (kushoto) akiwa na mama wa taifa nchini Poland Agata Kornauser-Duda