Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mwanamuziki Bobi Wine akamatwa Uganda
Mwanamuziki ya nyimbo za reggae nchini Uganda Robert Kyagulanyi, ambaye ni maarufu kama Bobi Wine, amekamatwa kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo.
Alikuwa akifanya kampeni kama mgombea huru kwa nafasi inayong'ang'aniwa vikalia nje ya mji wa Kampala, kwenye uchaguzi mdogo ambao utafanyika siku ya Alhamis.
Magazeti ya New Vision na Monitor yanasema kuwa hakukutolewa sababu ya kukamatwa kwake.
Lakini lile la Monitor linasema kuwa wafuasi wake walipambana na wale wa mpinzani wake jana Jumatatu.
Rais Museveni wa chama cha NRM na hasimu wake wa muda mrefu Dr. Kizza Besigye wa FDC, pia na wanatarajiwa kufanya mikutano eneo hilo leo, kuwaunga mkono wagombea wao.